Jumapili, 1 Februari 2015

DOLA LA KIISLAMU LAUA MWANDISHI WA HABARI



Wanamgambo wa itikadi kali wa dola ya kiislam-IS wadhihirika wamemuuwa  pia habusi wa pili wa Japan.Wamechapisha kanda ya video kupitia mtandao wa internet,inayoonyesha mwandishi habari Kenji Goto amekatwa kichwa.

Waziri wa ulinzi wa Japan Gen Nakatani amesema kanda hiyo ya video inaonyesha ni ya kweli.Katika kanda hiyo ya video anaonekana mtu aliyeficha uso wake akimuonya waziri mkuu wa Japan Shinzo Abe "jinamizi limeshanza kuikaba Japan." 

Serikali mjini Tokyo ilitangaza kati kati ya mwezi uliopita wa january kutenga  dala milioni 200 kama msaada ambao si wa kijeshi kwaajili ya mapambano dhidi ya wanamgambo wa IS.Waziri mkuu Abe ameshasema hawatoupigia magoti ugaidi.

Rais Barack Obama wa Marekani amelaani kitendo hicho kuwa ni cha kinyama.Katibu mkuu wa Umoja wa mataifa Ban Ki-Moon amelaani "mauwaji ya kishenzi" ya Goto na kuwataka wafuasi hao wa itikadi kali wawaachie huru haraka mahabusi wote wanaowashikilia.Jordan pia imelaani vikali kuuliwa mwandishi habari wa pili wa Japan Kenji Goto.
CHANZO: DW

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni