Ijumaa, 12 Desemba 2014

NORTHERN HIGHLANDS TEACHERS COLLEGE, HAPAFAI!!!!



U
salama wa wanafunzi wanaosoma katika chuo cha ualimu cha Northern Highlands Teachers College mjini Moshi upo mashakani kutokana na hofu ya kuangukiwa na miti iliyoshikizwa katika jengo hilo .
 Muonekano wa jengo la chuo cha ualimu cha Northern Highlands mjini Moshi, upande wa mbele


Wakizungumza, wanafunzi hao bila kutaja majina yao, wamedai kuwa, hofu ya usalama wao inatokana na ukweli kwamba,licha ya jengo hilo kutokamilika kwa aslimia 100, hadi sasa ndilo linalotumika kama madarasa na hapo hapo linatumika kwa ajili ya makazi yao.

Wamedai kuwa, Novemba 22 mwaka huu wanafunzi sita walilazwa katika Hospital binafsi ya Kilimanjaro iliyopo mjini hapa baada ya kupata mshituko uliotokana na kuanguka kwa moja ya tofari lililokuwa juu  ya jengo hilo na hivyo kuibua taharuki iliyosababisha wenzao kulazwa kwa siku mbili kwa matibabu.
Hata hivyo,katika kuficha ukweli,mmoja wa wakurugenzi wa Bodi ya chuo hicho, Henry Mallya, alikana kata kata kuwepo kwa tukio hilo ikiwamo wanafunzi hao kulazwa hospitalini lakini baada ya waandishi kuanza kupiga picha za jengo la chuo hicho,alianza kuwapigia simu na kuwasihi wasitoe habari za tukio hilo.

Mallya alikutana na waandishi wa habari mwishoni mwa wiki ofisini kwake iliyopo shule ya sekondari ya Norther Highlands ambako alikana kuwapo kwa tukio hilo, lakini baada ya nusu saa Mallya huyo huyo aliwapigia simu tena waandishi wa habari akiwasihi wasichapishe picha za jengo la chuo hicho baada yak upewa taarifa za wasaidizi wake juu ya picha hizo kupigwa.
Kwa mara ya pili Mkurugenzi  huyo ambaye pia anamiliki shule ya msingi ya The Moshi Academy, aliwaita waandishi wa habari kwenye ofisi yake iliyopo kwenye majengo ya shule hiyo ya msingi na kuwasihi wasichapishe habari au picha za chuo hicho akihofia ushindani wa kibiashara na licha ya kuelezwa kuwa waandishi wa habari hawafanyi biashara, alisisitiza kutochapishwa kwa habari hizi.

Maoni 1 :

  1. pole sana wanaosoma hapo na kweli ni hatari kwa usalama jitihada za maksudi zifanyike kabla ya madhara

    JibuFuta