Jumanne, 16 Desemba 2014

THIERRY HENRY ASTAAFU SOKA



Mshambuliaji wa zamani wa Ufaransa Thierry Henry amestaafu kandanda la kulipwa baada ya miongo miwili na sasa atakuwa mchambuzi wa kandanda kwenye televisheni ya Sky Sports nchini Uingereza.

Henry (Anri) mwenye umri wa miaka 37, alishinda Kombe la dunia na la Ulaya akiichezea timu ya taifa ya Ufaransa, na pia ndiye mfungaji wa magoli mengi zaidi katika klabu ya Arsenal kwenye Ligi Kuu ya England akiwa na mabao 226 katika mechi 370.

Kocha wa Arsenal Arsene Wenger alisema hivi karibuni kuwa Henry "bila shaka" atajiunga tena na klabu hiyo katika wadhifa mwingine katika siku  za usoni.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni