Jumatano, 17 Desemba 2014

GARI LA BENKI YA NMB LAKAMATWA KWA AMRI YA MAHAKAMA

G
ari aina ya Toyota LandCruiser lenye namba za usajili T394BVJ,linashikiliwa na Kampuni ya udalali ya Independent Agencies ya mjini hapa ili kurejesha fedha za mteja wa benki hiyo sh,Milioni 15,500,000 aliyeuziwa shamba na nyumba iliyopo katika mgogoro wa kifamilia.

Benki hiyo kupitia kampuni ya Udalali ya Mwafrica Group LTD inadaiwa kumuuzia nyumba  mteja huyo,Efrem Isaack Joseph  iliyopo katika kijiji cha Mdawi kata ya Kimochi wilaya ya Moshi vijijini may 18 mwaka huu  huku ikifahamu kuwa eneo hilo linao mgogoro.

Uamuzi wa kukamatwa mali za benki hiyo ili kurejesha fedha hizo ulitolewa wiki iiyopita mjini hapa na Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi la Nyumba wilaya ya Moshi,Muhelele Sukumba baada ya kukubaliana na madai ya mteja huyo kupitia kwa wakili wake David Shilatu .

Mteja huyo alifungua shauri  katika baraza hilo  akidai kutapeliwa na benki hiyo baada ya kumuuzia shamba lenye mgogoro huku akiiomba mahakama ya usuluhishi wa masuala ya Ardhi na Nyumba kuiamuru benki hiyo kumrejeshea fedha zake ama kumkabidhi mali yake huku pia akitaka alipwe fidia .

Hatua hiyo ilitokana na benki hiyo kumpa mkopo mteja wake  Adam Gard Moshi wa sh,Milioni na kuweka dhamana eneo hilo ambalo baadaye wazazi wake walijitokeza na kupinga uuzwaji wa shamba hilo kwa madai kuwa si mali ya mdeni wa benki hiyo.

Familia hiyo nayo ilifungua shauri katika baraza hilo kupinga uuzwaji wa shamba hilo na nyumba ambako baada ya ushahidi kuwasilishwa mbele ya baraza hilo,uuzwaj huo ulitenguliwa na shamba hilo kurejeshwa mikononi mwa familia.

Kutokana na kuwapo kwa mgogoro huo,benki hiyo ilishindwa kumkabidhi mteja huyo eneo hilo na hivyo kulazimika kuomba msaada wa kisheria kupata haki yake kutokana na kutishiwa  usalama wake muda mfupi baada ya maofisa wa benki hiyo kwenda kumkabidhi eneo hilo.

Kwa upande wake meneja wa NMB tawi la Nelson Mandela mjini hapa,Emmanuel Bushiri alikiri kukamatwa kwa gari hilo alipozungumza na blog hii mwishoni mwa wiki na kuongeza kuwa hilo lilitokana na baraza kujiridhisha kuwa taratibu za mnada zilikiukwa.

Alitaja baadhi ya taratibu zilizokiukwa na kampuni ya udalali ya Mwafrica kuwa ni pamoja na kutolipa kodi manispaa,kutoshirikishwa viongozi wa serikali ya Kijiji cha Mdawi pamoja na familia ya mdaiwa aliyekopeshwa na benki hiyo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni