Jumatatu, 22 Desemba 2014

WALIMU WAKUU 16 WASHUSHWA VYEO, MATOKEO DARASA LA SABA



Walimu wakuu 16 wa shule za msingi mkoani Dodoma  wameshushwa vyeo baada ya kushindwa kuwajibika vyema.

Ofisa elimu wa mkoa, Juma Kaponda alisema hayo katika mkutano wa wadau wa elimu ulioandaliwa kwa ajili ya kutangaza matokeo ya darasa la saba.

Kaponda alisema walimu hao wakuu wanatoka katika shule za Mwiyendaje na Segara wilayani Chamwino na wengine wanane wanatoka wilayani Chemba.

Walimu wakuu wengine waliokumbwa na kadhia hiyo ni wa shule za Kongogo, Mkakatika na Bankororo wilayani Bahi.

Katika Wilaya ya Mpwapwa walioshushwa vyeo ni walimu wakuu wa shule za Luhundiwa na Idiro.

Kaponda alisema Dodoma ilishika nafasi ya 21 kitaifa katika matokeo ya mtihani wa darasa la saba mwaka huu, wakati mwaka jana ulishika nafasi ya 23.

Hata hivyo, alisema takwimu zinaonyesha kuwa kiwango cha ufaulu kwa mwaka jana kilikuwa ni asilimia 38.2 (sawa na wanafunzi 15,053) na mwaka huu kimepanda na kufikia asilimia 45.3 (sawa na wanafunzi 16,672)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni