Jumapili, 4 Mei 2014

DIAMOND ANG'ARA TUZO ZA MUZIKI, AZOA SABA


Msanii wa kizazi kipya, Nasib Abdul a.k.a Diamond Platinumz Usiku ya Jana May 3, 2014 amedhihirisha kuwa yeye ni msanii mkali kwa kuchukua tuzo saba katika Tuzo za Kilimanjaro 2014 (KTMA).

Diamond amejinyakulia tuzo zifuatazo:-
Msanii Bora wa Kiume,
Video Bora ya Mwaka.
Mtumbuizaji bora wa Muziki wa Kiume.
Wimbo Bora wa Afro Pop.
Wimbo Bora wa Mwaka.
Mtunzi Bora wa mwaka Kizazi Kipya.
Wimbo Bora wa Kushirikisha/Kushirikiana.

Hakika Diamond ameonyesha ukali wake na kuonyesha kuwa yeye ni bora zaidi na anapendwa na watu.


Msanii Diamond Platnumz akipokea mojawapo ya tuzo zake 7 alizozipata katika Tuzo za Kilimanjaro 2014 (KTMA).

Mshindi wa tuzo  (7) za Kilimanjaro
Music Awards,
Diamond Platnumz akiwa
katika pozi na mpenzi wake
Wema Sepetu.


Aidha Huu ndio Mpangilio wote wa WASHINDI WOTE WA TUZO ZA KTM 2014,MEI 03:-.

Tuzo la Wimbo Bora Wenye Vionjo vya Asili vya Tanzania limeshindwa na… Bora Mchawi - Dar Bongo Massive.

Msanii Bora Chipukizi Anayeibuka ni Young Killer.

Wimbo Bora wa Zouk kwa 2014 ni... Yahya - Lady Jaydee.

Wimbo Bora wa Afro Pop ni Number One - Diamond Platinumz.

Kwa mwaka 2014, Wimbo Bora wa Ragga/Dancehall ni... Chibwa Ft. Juru – Nishai.

Wimbo Bora wa Reggae ni Niwe na Wewe – Dabo.

Wimbo Bora wa Taarab kwa mwaka huu ni... Wasi Wasi Wako-Mzee Yusuf.

Tuzo la Kikundi Bora cha Taarab limeshindwa na Jahazi Modern Taarab.

Mwimbaji Bora wa Kike - Taarab ni... Isha Ramadhani.

Mwimbaji Bora wa Kiume - Taarab ni... Mzee Yusuf.

Washindi wa Wimbo Bora wa Kiswahili Bendi kwa mwaka 2014 ni... Ushamba Mzigo - Mashujaa Band.

Mwimbaji Bora wa Kike - Bendi ni Luiza Mbutu.

Mwimbaji Bora wa Kiume - Bendi ni Jose Mara.

Rapa Bora wa Mwaka - Bendi ni Ferguson.

Tuzo la Bendi ya Mwaka limeshindwa na... Mashujaa Band.

Mwimbaji Bora wa Kike - Kizazi Kipya imeenda kwa... Lady Jaydee.

Mwimbaji Bora wa Kiume - Kizazi Kipya kwa mwaka huu ni... Diamond Platinumz.

Wimbo Bora wa R&B - Closer - Vanessa Mdee.

Kikundi cha Mwaka cha Kizazi Kipya ni... Weusi.

Wimbo Bora wa Hip-hop kwa mwaka 2014 imechukuliwa na... Nje ya Box - Nikki wa Pili Ft Joh Makini na Gnako.

Tuzo la Msanii Bora wa Hip-hop limeenda kwa... Fid Q.

Wimbo Bora wa Kushirikisha/Kushirikishana ni... Muziki Gani - Ney Mitego Ft. Diamond.

Wimbo Bora wa Afrika Mashariki - Jose Chameleone – Tubonge.

Mtunzi Bora wa Mwaka - Taarab... Mzee Yusuf.

Mtunzi Bora wa Mwaka - Bendi... Christian Bella.

Mtunzi Bora wa Mwaka - Kizazi Kipya imeenda kwa... Diamond.

Mtunzi Bora wa Mwaka - Hip-hop ni... Fid Q.

Mtayarishaji Bora wa Nyimbo wa Mwaka - Bendi – Amoroso.

Mtayarishaji Bora wa Nyimbo wa Mwaka - Kizazi Kipya ni... Man Water.

Hall of Fame - Individual - Rehan Bitchuka.

Hall of Fame - Institution - Masoud Masoud.

Video Bora ya Muziki ya Mwaka - Number One - Diamond Platinumz.

Wimbo wa Mwaka.... Number One – Diamond.

Mtumbuizaji Bora wa Kike wa Muziki... Isha Ramadhani.

Mtumbuizaji Bora wa Kiume wa Muziki... Diamond Platinumz.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni