Alhamisi, 15 Februari 2018

MTUMISHI MKOMBOZI BANKI AIBA MAMILIONI YA WATEJA,NAYE ALIZWA NA MATAPELI


 Na Charles Ndagulla,Moshi.

MTUMISHI mmoja wa benki ya kibiashara ya Mkombozi tawi la Moshi(jina tunalihifadhi),anatuhumiwa kuiba zaidi ya shilingi Milioni 57 kutoka kwenye akaunti za wateja wa benki hiyo.

Habari za uhakika ambazo mtandao huu umezipata zimedai kuwa,mtumishi huyo aliiba fedha hizo kati ya Oktoba na Desemba mwaka jana lakini polisi wameshikwa kigugumizi kuanika majina ya wateja waliolizwa fedha zao.

Taarifa kutoka ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali mjini Moshi,zinapasha kuwa,polisi wamekataa kuweka wazi majina ya wateja hao,akaunti zao na kiasi cha fedha kilichoibwa na mtumishi huyo.

Inadaiwa kuwa,kugoma kwa polisi kuweka majina ya wateja hao,kumeikwamisha ofisis hiyo ya mwanasheria mkuu wa serikali kuandaa hati ya mashitaka ili mtumishi huyo aweze kufikishwa makahamani.

Hata hivyo taarifa zinapasha kuwa,mtumishi huyo hakuweza kunufaika na mamilioni hayo ya wateja baada ya kuingizwa 'mjini' na matapeli waliomhadaa kuwa fedha hizo zitaongezeka mara dufu.

Kwa lugha nyepesi mtumishi huyo aliponzwa na uroho wa kupata utajiri wa chap chap bila kuutolea jasho na sasa yupo kikaangoni kwani anakabiliwa na tishio la kufukuzwa kazi wakati wowote.

Kwa taarifa zaidi juu ya sakata hilo enedelea kutembelea mtandao huu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni