Jumamosi, 19 Mei 2018

RUSHWA YA NGONO YATIKISA ARUSHA SERENA HOTEL



 Arusha Serena Hotel,Resort and Spa
 

 NA CHARLES NDAGULLA,ARUSHA

RUSHWA  ya ngono ni moja ya vitendo ambavyo vimekuwa vikiwakwaza wanawake katika  kupata ajira maeneo mbali mbali duniani hatua ambayo inatajwa kama moja ya changamoto kubwa katika mafanikio yao.

Kutokana na kukithiri kwa vitendo hivyo,wapo baadhi yao ambao licha ya kuwa na sifa za kuajiliwa wamejikutaka wakikosa fursa hizo kutokana na kushindwa kutoa rushwa ya ngono kwa wanaosimamia mamlaka za ajira.

Pamoja na  kelele ninyi kupigwa kutoka kwa watetezi wa haki za binadamu yakiwamo mashirika yasiyo ya kiserikali  juu ya kukithiri kwa vitendo hivyo,mambo bado yahajabadilika katika baadhi ya maeneo ya kazi hapa nchini.

Wafanyakazi wa kike katika Hotel ya kitalii ya Arusha Serena Hotel and Resort iliyopo kilometa 4.5 kutoka eneo la Tengeru nje ya Jiji la Arusha ni moja ya wahanga wa matukio hayo ya unyanyasaji wa kingono.

Wafanyakazi hao walioomba kutotajwa majina yao kwa sababu maalumu,wamezungumza na waandishi wa habari Jijini Arusha na kuelezea kilio chao juu ya vitendo hivyo ambavyo wanadai vinawakwaza katika utendaji kazi wao.

  
Kwa mujibu wa wafanyakazi hao,wamedai wengi wa wanaonyanyasika ni wafanyakazi wa kitanzania huku wafanyakazi kutoka nchini Kenya wakipewa huduma nzuri ikiwamo mishahara minono na maslahi mengine.
 Ndagullablog imezungumza na meneja Raslimali watu wa hotel hiyo John mwamakula juu ya malalamiko ya wafanyakazi hao kunyanyaswa kingono na baadhi ya maofisa wa hotel hiyo akiwamo meneja wake Filex Ongembo.

Katika mahojiano na Ndagullablog ofisini kwake wiki hii,Mwamakula hakukiri wala kukanusha malalamiko hayo huku akisisitiza vitendo hivyo ni kinyume na sera ya hotel hizo.

Amesema sera ya hotel hizo zilizopo maeneo mbali mbali nchini inakataza vitendo hivyo na kwamba anayebainika kufanya hivyo anakuwa katika hatari ya kufukuzwa kazi.

Mwamakula amesema kuwa hawajawahi kupokea malalamiko kutoka kwa wafanyakazi hao kunyanyaswa kingoni lakini akadai zipo njia tatu kwa wafanyakazi hao kuwasilisha malalamiko yao kwa uongozi.

Ametaja njia hizo kuwa ni pamoja na utoaji taarifa kwa njia ya siri(wisow blower),mfanyakazi kwenda moja kwa moja ofisini kwake na kupitia mikutano ya wafanyakazi(Staff General Meeting) ambayo amedai hufanyika kila baada ya miezi mitatu.

“Kwa ujumla hatukubaliani na hivyo vitendo na hata ukiangalia sera yetu inakataza vitendo hivyo na adhabu yake ni kali sana kama ikibainika mtu amehusika na vitendo hivyo tunamfukuza kazi”,amesema.

Hata hivyo meneja huyo alipoulizwa alipo Ongembo amesema hajui alipo zaidi ya kusema hayupo na taarifa ambazo jamhuri limezipata ni kwamba meneja huyo amerejeshwa nchini kwao Kenya.

Malalamiko mengine ya wafanyakazi hao ni kupunguzwa kwa mishahara yao kwa aslimia tano tangu mwaka jana na meneja huyo amekiri kuwepo na punguzo hilo la mishahara kwa wafanyakazi hao.

Akijibu malalamiko hayo,Mwamakula amesema kuwa,makato hayo yalitokana na kuyumba kwa biashara ya utalii mwaka jana madai ambayo wafanyakazi hayo wameyapinga.

 Huduma ya matibabu ni moja ya malalamiko mengine kwa watumishi ambako wanadai mwajili wao kuwaondoa kwenye huduma ya matibabu kupitia bima ya Afya(NHIF) huku wakitibiwa kupitia bima ya Jubilee ambayo wamedai haiwapi nafasi ya kwenda kutibiwa katika hospital za rufaa.

Wametaja changamoto nyingine kuwa ni pamoja na kutopewa usafiri wa kutoka nyumbani kwenda kazini na kurudi majumbani hali ambayo imewalazimu kutumia zaidi ya shilingi 10,000 kwa siku kama gharama za usafiri fedha ambazo wanadai zinazotoka kwenye sehemu ya mishahara yao.

Licha ya kutopewa usafiri,wafanyakazi hao wamedai kuwa usalama wao uko shakani kutokana na kutumia usafiri wa boda boda usiku wa manane wakati wa kutoka kazini kutokana na boda boda wengi kutowafahamu.

“Tunaomba mtusaidie kwa kweli hali ni mbaya,wafanyakazi wa kitanzania tunanyanyasika sana tofauti na wenzetu wakenya ambao wanaishi vizuri licha ya baadhi yao kutokuwa na hadhi ya kufanyakazi ambazo tunauwezo nazo”,wamesema.

Hata hivyo wafanyakazi hao wamedai  kuwa,wamekuwa katika tishio la kufukuzwa kazi pindi wanapodai kuboreshewa mazingira ya kazi hatua ambayo imewafanya baadhi yao kukaa kimya kwa hofu ya kufukuzwa kazi.

Wafanyakazi hao wameitaka wizara ya kazi,ajira na vijana  pamoja na idara ya uhamiaji Jijini Arusha kufanya uchunguzi wa kina kwa baadhi ya wafanyakazi wa hotel hiyo kutoka nchini Kenya kwani baadhi yao hawana sifa za kufanyakazi hapa nchini.

“Ukienda pale ofisi kuu utawakuta wakenya wamejazana pale wengine hawana sifa za kuwa hapa nchini kwa sababu baadhi ya kazi wanazofanya hazihitaji watu kutoka nje ya nchi,wapo wanafanyakazi kama makatibu mhitasi,je kazi hiyo inahitaji mtu kutoka Kenya?,wamehoji.

  Kuhusu suala la matibabu,Mwamakula amesema kuwa si kweli bima ya Jubilee inawanyima fursa ya kutibiwa katika Hospital za rufaa huku akikiri kujiondoa katika Bima ya Afya ya NHIF.

“Mpango wetu wa matibabu unagusa mfanyakazi na mwenza wake kama ameoa ama kuolewa na watoto wasiozidi wanne wenye umri chini ya miaka 18”,amesema.

Amesema wafanyakazi hao pia ni wanachama wa mfuko wa hifadhi ya Jamii (NSSF) ambako kuna  mpango wa matibabu kupitia fao la matibabu ambako mwanachama anaweza kujiandikisha bila kuathiri michango yake na akachagua Hosptil anayoitaka.

Mbali na huduma hizo,meneja huyo amesema wafanyakazi hao wanayo bima nyingine ambako matibabu yakishindikana hapa nchini wanaweza kupelekewa nchini Kenya kwa matibabu zaidi.

Maoni 4 :

  1. Jamani wakenya wameshatuchosha kabisa sio hata Serena tu, mahotel mengi watanzani wamekuwa wakionwa kama mambwa mwitu ndugu zangu. Wamekuwa wakilipwa mishahara mingi lakini watenda kazi walio wengi ni watanzania, ukilinganisha mshahara Wa mtanzania hata robot ya mahitaji yake ya mwezi haufiki, as kama watanzania tu naomba sana haya mashirika ya kazi yatembelee hizi hotel, tunateseka jamani watu hawana overtime wala nn

    JibuFuta
  2. Marandu nakushukuru kwa maoni yako,tunajipanga kuwasiliana na waziri mwenye dhamana na ajira tumfikishie hayo malalamiko,yapo mengi sana kwa kweli na kama ulivyosema si serena pekee,hivyo tukimpata waziri mwenye dhamana tutafanya naye mahojiano na kupata msimamo wa serikali,naomba nikutakie siku njema na uendelee kutembelea blog yetu na usisite kutoa maoni yako.

    JibuFuta
  3. Safi sana Ndagulla keep it up.

    JibuFuta
  4. Thanks For Information.

    Best Hotels in Arusha

    http://www.crestsafarilodge.com/

    Crest Safari Lodge is the perfect choice, if you are in search of Budget Hotels. Crest Safari Lodge is one of the Best Hotels in Arusha, just right for Camping and Cultural Tours.

    JibuFuta