Alhamisi, 4 Januari 2018

URAIA WA MCHUNGAJI WA KANISA LA YESU ANAWEZA MOSHI UTATA


Na Charles Ndagulla,Moshi.

MCHUNGAJI Zakaria Donald Yona wa Kanisa la Yesu Anaweza Centre ameingia matatani akituhumiwa kuishi nchini isvvyo halali  baada ya kudaiwa kuwa ni raia wa Kenya.

Uchunguzi wa mtandao huu  umebaini kuwa,mchungaji huyo ni raia wa Kenya kwa kuzaliwa lakini mwenyewe amekana tuhuma hizo na kudai  ni mtanzania kwa kuzaliwa.

Kwa mujibu wa nyaraka ambazo mtandao wa NdagullaBlog umeziona zinaonyesha kuwa,mchungaji huyo anayeendesha kanisa lake eneo la Mji Mpya Manispaa ya Moshi,alizaliwa mwaka 1964  eneo la Siaya mkoa wa Nyanza nchini Kenya.

Kulingana na nyaraka hizo,baada ya kuzaliwa alipewa cheti chenye namba ya ingizo 4300247/85  akitambuliwa kwa majina ya Donald Oloo Waswani huku pia akiwa na kadi ya utaifa wa Kenya yenye namba 237104963 iliyotolewa Oktoba 10 mwaka 2013.

Pia mke wa mchungaji huyo anayetumia majina ya Redempter William Francis kwa hapa nchini,uchunguzi umebaini kuwa alizaliwa mwaka 1970 huko Machakos nchini Kenya huku akiwa na kadi ya uraia wa nchi hiyo yenye namba 223854431 iliyotolewa mwaka 2007.

Uchunguzi zaidi  umebaini kuwa,mchungaji huyo amesajiliwa kama mlipa kodi na mamlaka ya mapato nchini Kenya(KRA) na kupewa namba ya utamburisho wa mlipa kodi(Personal Identification Number) Na A.010329470.

Mchungaji huyo na mkewe Redempter William Francis,wanadaiwa kufunga ndoa yao Oktoba 13 mwaka 1991 katika Kanisa la Dandora Gaspel Tabernacle na kupewa cheti chenye namba 465369.

Hata hivyo mchungaji huyo amezungumza na NdagullaBlog  na kutupilia mbali tuhuma hizo lakini akishindwa kuweka wazi ni wapi  alipozaliwa akidai wakati ukifika ataweka wazi kila kitu.

“Suala la mimi nimezaliwa wapi tutakuja kuliweka sawa lakini kwa ufupi mimi ni mtanzania kwa kuzaliwa na hayo mengine yote yatajulikana huko mbele ya safari”,alisema .

Wakati mchungaji huyo akikwepa kuweka wazi alikozaliwa,NdagullaBlog imefanikiwa kuona nyaraka mbalimbali baadhi zikidaiwa ni za kughushi zikionyesha mchuangaji huyo alizaliwa Nyamagana mkoani mwanza mwaka 1964.

Kwa mujibu wa cheti cha kuzaliwa kilichosajiliwa Machi 15 mwaka 2010,kinaonyesha mchungaji huyo alizawali eneo hilo na kusajiliwa kwa jina la Zacharia Donald Yona Munuo.

Pia mkewe ambaye kwenye cheti cha kuzaliwa nchini Kenya anatumia majina ya Redempter Ndinda Nthenge,kwenye cheti cha kuzaliwa hapa nchini anatambulika kwa majina ya Dedempter William Francis Munuo akidai alizaliwa Nyamagana mkoani Mwanza mwaka 1969.

Wawili hao pia wanadaiwa kufunga ndoa ya kiserikali mkoani Kilimanjaro Juni 13 mwaka 2007 na kupewa cheti  B/N na.0748488 hali ambayo inazidisha utata zaidi juu ya uraia wa wawili hao.

Mchungaji huyo amekiri kuwahi kukamatwa yeye na familia yake yote na maofisa wa jeshi la uhamiaji mkoani Kilimanjaro na kufikishwa makahamani akidaiwa kuishi nchini isivyo halali.

“Tulikamatwa juni 20 mwaka jana na wakatushikilia kwa siku mbili na baadaye wakatupeleka mahakamani,madai yao ni kwamba mimi na familia yangu si raia wa Tanzania bali ni raia wa Kenya”,amedai.

Amedai kuwa,uhamiaji walidai kuwa wangepeleka mashahidi 15 na vielelezo zaidi ya 20 kudhibitisha kuwa mchungaji huyo si raia wa Tanzania lakini hawakufanya hivyo.

Hata hivyo mchungaji huyo amesema kuwa,uhamiaji waliondoa shauri hilo mahakamani  desemba 6 mwaka jana baada ya kudai upande wa jamhuri hauna nia tena ya kuendelea kuwashitaki.

Mchungaji huyo amedai kuwa,wakati wakiamini suala hilo limeisha na wako huru kuendelea na maisha yao,walijikuta wakikamatwa tena nje ya mahakama na kupelekwa ofisi za uhamiaji .

Kwa mujibu wa mchungaji huyo,baada ya kufikishwa katika ofisi hizo walilazimishwa kusaini nyaraka za kuondolewa nchini na walipokataa kusaini nyaraka hizo waliondolewa nchini kwa nguvu na kupelekwa mpaka wa Tanzania na Kenya eneo la Holili.

“Tulipofika holili maofisa wa uhamiaji wa Kenya walikataa kutupokea baada ya uhamiaji Tanzania kukosa nyaraka mhimu kuonyesha sisi hatutakiwi Tanzania zikiwamo nyaraka za mahakama”,amesema.

Mchungaji huyo amesema kuwa  baada ya zoezi hilo kugonga mwamba,maofisa hao wa uhamiaji waliamua kuwatelekeza mpakani na kuondoka kabla ya mchungaji huyo na familia yake kuamua kurejea  nyumbani kwa kutumia usafiri mbadala.

Msemaji wa uhamiaji mkoani Kilimanjaro(DCI),Albert Rwelamila amedhibitisha kuwepo na uchunguzi unaofanywa na ofisi yake juu ya uhalali wa uraia wa mchungaji huyo na familia yake alipozungumza na NdagullaBlog hivi karibuni.

Hata hivyo,Rwelamila hakuwa tayari kulizungumzia suala hilo kwa undani zaidi kwa kile alichodai lipo zuio la mahakama kuu linalowataka kusitisha mchakato huo hadi hapo suala hilo litakapotolewa uamuzi.

“Ni mhimu tukaheshimu zuio la mahakama maana ni chombo cha kisheria nadhani baada ya kusikiliza pande zote na kutoa uamuzi hapo tunaweza kuwa na cha kusema,kwa sasa tuliache kwanza”,alisema.

NdagullaBlog imeambiwa kuwa,zuio hilo limewekwa baada ya mchungaji huyo kukimbilia mahakama kuu desemba 15 mwaka jana kupitia kwa wakili wake Caessar  Shayo.

Kwa upande wake wakili Shayo amesema kuwa  hati ya zuio ilitolewa desemba 18 mwaka jana na Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Kanda ya Moshi,Aishiel Sumari.



Maoni 1 :

  1. SAFARI YAKO YA MAFANIKIO UTAJIRI NA RIZIKI ZAKO ZIMESIMAMA NA KUZINASUA UWEZE KUSONGA MBELE SOMA KWA UMAKINI UWEZE KUIJUA SIRI HII.

    KATIKA SAFARI YA MAFANIKIO TUNAPITIA MENGI ILI TUWEZE KUFANIKIWA LAKINI WENGI WETU KUNA MAMBO MACHACHE SANA WENGI WETU TUNAYADHARAU NA KUMBE NDIO CHANZO CHA MAFNIKIO YETU.

    N.B KWA WALE WAHITAJI WA PESA ZA NDAGU au MAJINI kwa mudamfupi nipigie DOKTA MDIRO +255 742162843
    MALIPO NI BAADA YA KUFANIKIWA PIA UMBALI POPOTE ULIPO KENYA,UGANDA, OMAN, CONGO RWANDA N.K
    WOTE NAWAKARIBISHA.

    (kuhusu utajiri au pesa) KABLA YA KUPIGA SIMU ZINGATIA YAFUATAYO
    1. uwe una umri wa miaka 18+
    2. uwe tayari kupokea masharti yote
    3.uwe na uwezo wa kutunza siri
    4. uwe jasiri wa kupokea taarifa yoyote
    KARIBU SANA KWA SHIDA NYINGINE PIA ULIYONAYO AMBAYO SIJATAJA INSHAALAH ITATATULIWA IKIWA NDANI YA UWEZO WANGU.(HUSITUME SMS PIGA SIMU KUHEPUKA MATAPELI)

    HAYA NI MAMBO 7 YAKUZINGATIA KATIKA SAFARI YAKO YA MAFNIKIO

    i) Wazazi wako wakiwa wamekulea mpaka ukawa mkubwa wafumbua macho unawaona akikisha usiwafanye wakajuta kukuzaa asilimia kubwa wazazi wanakuwa na tabu sana ila zile tabu zao ndio zinazokufanya wewe una aminiwa na watu na unaeshimika na kujieshimu

    Kwaiyo jitahidi sana kuwa nao vizuri kuna wengi maisha yao wanaishi kwa shida chanzo ni utofauti baina ya wazazi wao

    Ukiona wazazi wako wanatabu sana usiwajibu vibaya wewe kaa nao mbali ila wape majukumu yao unacho fanya kuwaona nakurudi ulipo apo utaona mambo yako yatakuwa vizuri sana

    ii) JAMBO LA PILI
    Akikisha unatunza uzao wako yani ukijua ni mtoto ni wako basi jitahidi sana kutoa uduma ata kidogo ulicho nacho lakini udumia usiache uzao wako unateseka na njaa wewe una kula maisha aisee fahau

    Kila mtoto wako anavyo kuwa ndio mambo yako yanaaribika usipo udumia kwaiyo ukiwa waitaji kufanikiwa zaidi jali uzao wako

    iii) JAMBO LA TATU
    ukiwa umeoa au umeolewa usitoe talaka au kuomba talaka kabla mwenzio ayupo tayari kwa muda huo fahamu ukiomba talaka au akikupa talaka bila bila sababu ya msingi yeye tu ana matamanio ya kidunia basi anamuda atapoteza muelekeo wa maisha yake

    iv) UKIWA WAPATA PESA
    ukiwa wapata pesa alafu utoi sadaka basi kufikia kwenye ukuu utachelewa sana mana mana pesa badala ya kutoa kwa iyari yako utatoa kwa matatizo kwaiyo jitahidi icho icho kidogo toa sadaka kwa wenye uitaji

    v) USIMZULUMU MTU
    kama wataka kufika mbali kwenye mafanikio yako usimzulumu mtu ata kwa uchache wa kitu usifanye ivyo itakugarimu kiasi kikubwa

    vi) USIZARAH MILA
    ukiwa kwenu kuna mambo ya mila mzimu tambiko jitahidi kufatilia sana aya mambo yanarudisha nyuma sana usipo yawahi mapema

    vii)USIWE WA NAMNA
    1)ikiwa ujafanikiwa jitahidi sana usiwe mvivu kufanya kazi usiwe muhuni usiwe mwenye chuki na asira zisizo za msingi usiwe na tamaa nyoa vizuri vaa nguo za eshima na usiige maisha ya watu.

    KWA MAWSILIANO ZAIDI KUHUSU MATATIZO MBALIMBALI YA TIBA ASILI NA TIBA MBADALA, PETE MALI ZA NDAGU NA MAJINI N.K

    DOKTA MDIRO Call/whatsup +255 742162843.

    JibuFuta