Alhamisi, 6 Novemba 2014

UVAMIZI MAPITO YA WANYAMA HIFADHI YA TARANGIRE, WATISHIA UHAI WA WANYAMA



H
ifadhi  ya Taifa ya Tarangire ilianzishwa mwaka 1970 kwa tangazo la serikali namba 160 lengo likiwa ni kuhifadhi makimbilio ya wanyama wakati wa majira ya kiangazi.
 
Malengo mengine ya kuanzishwa kwa hifadhi hiyo ni kuhifadhi maeneeo ya mto Tarangire unaobeba jina la hifadhi hiyo pamoja na ardhi oevu ambayo ni chanzo pekee cha maji wakati wa majira ya kiangazi.

Inaaminika kwamba,kipindi hicho cha kiangazi ndicho kipindi ambacho wanyama kunakuwapo na mkusanyiko mkubwa wa wanyama katika eneo la hifadhi.

Wanyama hao  huhama ndnai ya hifadhi hiyo kuelekea masahriki,kaskazini na kusini kwa ajili ya malisho na kuzaliana hususani wanyama kama nyumbu na pundamilia katika miezi ya Oktoba na Novemba ambayo ni kipindi cha masika.

Pamoja na umhimu wa hifadhi hiyo kuichumi kutokana na kuwa moja ya hifadhi tano zinazozalisha ziada,kumekuwapo na changamoto nyingi zinazochanhgia kukwaza shughuli za uhifadhi.

Mkuu wa hifadhi hiyo(CPW),Stephano Qolli,anasema moja ya changamoto zinazokwaza shughuli za uhifadhi ni tishio la kutoweka kwa wanyama kutokana na kuvamiwa kwa mapito yao kutokana na shughuli za kibinadamu.

Anasema kasi ya ongezeko la idadi ya watu na matumizi ya ardhi litaifanya hifadhi hiyo kuwa kisiwa  endapo hatua za makusudi hazitachukuliwa katika kuyalinda mapito hayo ya wanyama.

Katika taarifa yake kwa kamati ya kudumu ya Bunge ya Ardhi,maliasili na mazingira,Mkuu huyo wa hifadhi anasema kuwa,kuna hatari hifadhi hiyo ikatenganishwa na maeneo ya mazalio ya wanyama na mlisho.

Alionya kuwa,wanyama hao wanaweza wakapungua ama kutoweka kabisa endapo maeneo hayo ya malisho yataharibiwa  kutokana na ongezeko kubwa la shughuli za kibinadamu.

Aliwaambia wajumbe wa kamati hiyo kuwa,katika kukabiliana na changamoto hizo,hifadhi imekuwa  ikitoa elimu kwa wananchi na wadau mbalimbali pamoja na kusaidia mradi wa mpango wa mtumizi bora ya ardhi hususani katika vijiji jirani.

Tishio la kuharibiwa vyanzo vya mto Tarangire

Pamoja na tishio la kutoweka  kwa wanyam katika hifahdi hiyo kutokana na kuvamiwa kwa mapito yao,shughuli za kibinadamu ikiwamo kilimo,ufyekaji misitu na ufugaji vimedaiwa kuathiri vyanzo vya maji katika mto tarangire.

Kwa mujibu wa mhifadhi huyo,mto tarangire unaanzia katika milima ya kondoa takribani kilometa 50 kusini mwa hifadhi hiyo ambapo mbali na milima hiyo ya kondoa,pori la akiba la mkungunero nalo ni mojawapo ya chanzo.
Anasema pori hilo pamoja na sehemu ya kusini nalo limevamiwa na mifugo mingi huku shughuli kubwa za kilimo zikiendelea kwa kasi hali ambayo inaweza kuhatarisha uwepo wa hifadhi hiyo.

"tatizo hili linahitaji uelimishwaji wa jamii pamoja na utatuzi wa migogoro ya mipaka kati ya vijiji na maeneo yaliyohifadhiwa na kati ya mikoa ya dodoma na manyara",anasema.


Migogoro ya mipaka

Migogoro ya mipaka ndani ya hifadhi za taifa na misitu ya hifadhi ya taifa limekuwa ni tatizo sugu na ambalo kwa hakika bado halijapatiwa ufumbuzi wa kina na mamlaka husika.

Hali hiyo imeleta misuguano ya mara kwa mara baina ya ungozi wa hifadhi husika kwa upande mmoja na wananchi wanaoishi kuzunguka maeneo hayo ya hifadhi kwa upande wa pili.

Vivyo hivyo hifadhi ya taifa ya tarangire nayo hasijaachwa nyuma katika migogoro hiyo ambko mpaka sasa upo mgogoro unaofukuta katika kijii cha Kimotorok kinachopakana na hifadhi hiyo.

Kijiji hicho kipo wilaya ya Simanjiro lakini mpaka wa kijiji hicho umevuka mpaka wa wilaya na kuingia wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma hivyo utatuzi wake unahitaji ushirikiano wa mikoa hiyo miwili.

Kwa mujibu wa mhifadhi huyo,wananchi wa kijiji hicho hawautambui mpaka wa kijiji kama unavyoonekana katika ramani ya mwaka 1993 huku pia wakikataa kuutambua mpaka wa hifadhi baada ya kuhakikiwa mwaka 204.

Wananchi hao pia wanadaiwa kutolitambua pori la akiba la Mkungunero kwa madai kuwa hawakushirikishwa katika uanzishwaji wake na pia hawautambui mpaka uliopo kati ya mkoa wa Dodoma na Manyara.

Mhifadhi huyo anasema kuwa,endapo eneo hilo   litabaki kwa shughuli za kibinadamu,hifadhi ya tarangire na pori la akiba la Mkungunero zitakuwa
zimetenganishwa.

Anasema kuwa kutenganishwa huko kutaleta athari kubwa kimazingira na kiikolojia ikiwamo kufungwa kwa mapito ya wanyama ambako mapato yatokanayo ya utalii yatapungua.

Ametaja athari nyingine kuwa ni pamoja na uharibifu wa mazingira utakaotokana na kuongezeka kwa shughuli za kibinadamu ikiwamo mifugo,kilimo na makazi hivyo kuathiri mtiririko wa mto Tarangire.

Ngoma ya asili  ikichezwa katika uzinduzi wa mradi wa wa majengo ya vyumba vya madarasa katika shule ya msingi ya Sangaiwe mkoani Manyara uliofanywa na mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge,Ardhi,Maliasili na Mazingira,James Lembeli hivi karibuni

Imetayarishwa na:
Charles Ndagulla
+255-(0)-783 847 877

Jumatatu, 3 Novemba 2014

MTANZANIA ATESWA DUBAI


 MWANAISHA ATHUMANI PINDE

Usalama  wa watanzania wanaopelekwa nchini Dubai  na Falme za Kiarabu kujaribu fursa za ajira upo shakani kutokana na baadhi ya waajiri nchini humo kuwafanyia vitendo visivyokuwa vya kibinadamu ikiwamo kupokwa pasi zao za kusafria na wengine kujikuta wakiswekwa jela bila hatia.

Uchunguzi uliofanywana mtandao huu kwa zadi ya mwezi mmoja sasa umebaini kuwa mbali na hilo,watanzania hao wamejikuta wakifanya kazi kwa mali kauli pasipo kulipwa mishahara yao kama ambavyo mikataba ya ajira inavyoosha.


Mmoja wa wahanga hao ni binti mwenye umri wa miaka 36 ,Mwanaisha Athuman Pinde aliyezaliwa mkoani  Morogoro Novemba 25 mwaka 1978 kama pasi yake ya kusafiria inavyoonyesha.

Kwa mujibu wa nyaraka tulizonazo,Mwanaisha aliondoka Jijini Dar e s salaam kwenda Dubai  Februari 17 mwaka huu na ndege ya shirika la ndege la Qatar yenye namba QR1350.

Uchunguzi umebaini kwamba alisafiri kwa msaada wa kampuni ya Bravo Job Centre Agency Ltd ya Jijijini Dar es salaam inayojihusisha na kuwatafutia fursa za ajira watanzania katika nchi mbalimbali na kupokelewa na wakala aitwaye Oriental Int,Labour Supply aliye na mkataba na Bravo.

Habari zinadai kuwa,baada ya binti huyo kupokelewa na kupelekwa kwa mwajili wake,alijikuta akiingia kwenye mgongano na mama mwenye nyumba na kulazimika kusitisha mkataba na kupelekwa kwa mwajili mwingine.

Kwa mujibu wa dada wa binti huyo,Zena Athuman Pinde,mdogo wake huyo baada ya kupelekwa kwa mwajili mwingine aliipokwa pasi yake ya kusafiria,simu pamoja na nyaraka nyingine huku akinyimwa kufanya mawasiliano na ndugu zake.

Zena alisema kuwa,mbali na hilo mdogo wake alikuwa akiishi bila kulipwa mshahara na pale alipodai mshahara wake alijikuta akiambulia lugha chafu kutoka kwa mwajili wake.

Kwa upande wake Mwanaisha akiongea na mwandishi wa habari hizi  kwa njia ya simu kutoka Abu Dhabi hivi karibuni,alisema alijikuta akiswekwa jela na maofisa wa polisi wa huku baada ya mwajili wake kumtelekeza na kushidwa kumrejesha nyumbani huku pasi pake akiwa ameishilikia pamoja na simu yake ya kiganjani.

Akizungumza kwa msaada wa ofisa wa polisi mwenye asili ya Tanzania,mwanaisha amedai kuwa,chanzo cha kutofautiana na mwajili wake ni hatua ya bosi huyo kutaka kumgeuza kitega uchumi kwa kumbadilisha kazi za ndani na kutaka kumtumia katika biashara haramu.

Amedai baada ya kugoma,alijikuta katika mgogoro na bosi wake na hapo upepo ukawa mbaya kwake kwani alijikuta akipokwa kila kitu huku akiwa hajalipwa mshahara wake kwa muda wa miezi sita sasa.

kwa mujibu wa mwanaisha,tangu awasili Abu Dhabi,amekuwa hana mawasiliano na ndugu zake kutokana na simu yake kuwa mikononi mwa bosi wake japo amefanikiwa kurejea nyumbani kwa msaada wa ubalozi mdogo wa tanzania huko Abu Dhabi baada ya kupatiwa hati ya muda ya kusafiria.

Akizungumza muda mfupi baada ya kurejea nchini hivi karibuni na ndege ya shirika la ndege la kenya na kupokelewa na ndugu zake,mwanaisha anadai kwa sasa anakamilisha tararibu za kisheria kuifikisha mahakamani kampuni ya Bravo kwa kile alichodai kushindwa kumsadia kupata haki zake.

Hata hivyo,msemaji wa kampuni hiyo ya Bravo,Heri Mtemvu akizungumza na mtandao huu hivi karibini ofisini kwake Keko Bora jijini Dar es salaam,alitetea hatua ya waajili huko Dubai ya kuwapoka simu na pasi za kusafiiria watanzania wanaokwenda kufanya kazi huko.

Kwa mujibu wa Mtemvu,hatua ya kupokonywa pasi na simu ni katika juhudi za kuzima majaribio ya watumishi hao kutoroka pindi wanapopata vibali vya kuwawezesha kufanyakazi nchini humo.

Mtemvu hata hivyo alisema,kampuni yake ipo katika hatua za mwisho kwenda nchini Dubia kufuatilia haki za mtanzania huyo ikiwamo mishahara yake pamoja na pasipoti yake ya kusafiria ambayo ingali mikononi mwa tajili yake.

Kwa mujibu wa nyaraka tuliozonazo,safari za watanzania kwenda katika nchi za falme za kiarabu zimekuwa zikipata baraka kutokana wakala wa Huduma za ajira Tanzania(TaESA) ambako mhusika hulipia ada ya sh,100,000 .

Nyaraka hizo zinaonyesha kuwa,mwanaisha alikuwa na mkataba  wa kufanyakazi za ndani kwa  mfanyabiashara Mohamed Saleh Yeslam Alameri ulioidhinishwa februari 5 mwaka huu na kutiwa saini na Omary Mjenga kutoka TaESA.

"mtajwa hapo juu mwenye pasipoti namba AB474488 amethibitishwa na ubalozi wa tanzania ulioko Dubia,UAE kwmaba amepata kazi nchini humo,wakala wa huduma za ajira tanzania umeridhia utaratibu uliotumika kwa kumuunganisha  mtajwa hapo juu na fursa ya ajira",inasema barua ya TaESA.

Barua hiyo iliyotumwa uhamiaji kwa taratibu zadi ya kiuhamiaji,ilisainiwa na K.V.Kilindu  februari 12 mwaka huu kwa niaba ya mtendaji mkuu wa TaESA huku ikiwa imebandikwa picha ya mwanaisha.

kwa mujibu wa mkataba ambao nakala yake tunayo,mwanaisha alikuwa alipwe mshahara wa AED 1100  sawa na sh,460,000 za tanzania lakini kwa mujibu wa maelezo yake,alielezwa kuwa atalipwa AED 800 sawa na sh,360,000 ambazo hata hivyo alidai hajawahi kulipwa.