Jumatano, 26 Novemba 2014

UVAMIZI VYANZO VYA MAJI UNACHANGIWA NA WATENDAJI WABOVU



Uvamizi  yanaofanywa na watu  kwenye vyanzo vya maji katika naeneo mbalimbali ya mji wa moshi yanatokana na matunda ya uongozi mbovu wa watendaji waliopewa dhamana ya kusimamia sheria za mazingira katika ofisi ya mkurugenzi wa Manispaa ya moshi.
MEYA WA MANISPAA YA MOSHI, JAPHARY MICHAEL
Tuhuma hizo zilitolewa  na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Moshi, Japhary Michael katika mkutano wake na waandishi wa habari uliolenga kuelezea hali halisi ya upatikanaji wa maji safi na salama kwa wakazi wa manispaa hiyo na changamoto zinazoikabili mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira moshi mjini(MUSWA).

Meya huyo alisema kuwa upo ulegevu katika suala zima la utekelezaji wa sheria ambao umesababisha watu kujenga karibu na vyanzo vya maji kikiwamo chanzo cha maji cha Njoro ya |Dobi ambacho katika miaka 15 iliyopita,chanzo hicho kilikuwa moja ya vyanzo mhimu vya maji katika mji wa Moshi.

Alisema kuwa chanzo hicho kimevamiwa na watu  na kuweka makazi ya kudumu licha ya kelele za watetezi wa mazingira na kuongeza kuwa uvamizi huo umechangiwa na wenye mamlaka ya kusimamia sheria kutokuchukua hatua stahiki.

Kwa sasa chanzo hicho cha maji hakitumiki kwa matumizi ya binadamu kutokana na kuvamiwa na wananchi waliojenga nyumba za makazi ambako wamekuwa wakitiririsha maji machafu yanayotokana na kinyesi cha binadamu hali ambayo imekiweka chanzo hicho katika mazingira hatarishi.

Kuhusu ujenzi holela unaoendela katika baadhi a maeneo ya mji wa moshi,mtahiki meya huyo alisema kuwa,ujenzi huo holela unashika kasi kutokana na usimamizi mbovu wa watendaji wa manispaa ya moshi ambapo shutuma hizo alizielekezam oja kwa moja kwa idara ya mipango miji ambayo ndiyo yenye wajibu wa kuhakikisha ujenzi holela unadhibitiwa.

Kuhusu hali ya upatikanaji wa maji katika mji wa moshi,meya huyo alisema kuwa,kwa sasa kuna jitihada kubwa zinazofanywa na MUWSA katika kutatua tatizo la maji kwa wakazi wam ji wa moshi huku maoneo yaliyokuwa yakikabiliwa namgao mkubwa wa maji kama vile Kiboriloni,Msaranga,pasua na Bomambuzi,maeneo hayo kwa sasa yanapata maji ya kutosha.

Hata hivyo, Meya huyo alisema kuwa,yapo baadhi ya maeneo ambayo bado hayapati maji ya uhakika na kwamba hiyo ni changamoto kwa MUWSA kuhakikisha maeneo hayo yanapata maji ya kutosha huku akielezea matumaini kwa wakazi wa kata za pasua na Bomambuzi ambao kwa sasa wananufaika na mradi wa maji kutoka chanzo cha maji cha mto karanga.

Alitoa wito kwa wakazi wa manispaa ya moshi kuwa mabalozi wazuri katika kusimamia ulinzi wa miundombinu ya maji ikiwamo pia kuwa na matumizi mazuri ya maji safi na salama na kuzuia upotevu huo wa maji.

Akizungumzia mfumo wa maji taka,meya huyo alisema kuwa bado jamii ya wananchi wa mji wa moshi hawajapata elimu ya kutosha juu ya kuunganishwa kwenye huduma hiyo na kuongeza kuwa hiyo ni changamoto kwa MUWSA na manispaa kutoa elimu kwa wananchi juu ya umuhimu wa kuunganishwa katika huduma hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa ya MUWSA, mji wa moshi umegaswanywa katika kanda kuu tisa ambako kila kanda inapata maji kwa wastani wa saa 18 hadi 24 kutegemea na eneo lilivyo ambako katika kipindi cha julai 2013 hadi sasa,wastani wa kutoa huduma ya maji kwa wateja umeimarika kutoka saa 17.3 hadi saa 21.5.

Alhamisi, 6 Novemba 2014

POLISI ALIYEMFUNGIA MWANAFUNZI GESTI ASHITAKIWA KIJESHI



J
eshi  la  Polisi nchini limemkamata na kumfungulia mashitaka ya kijeshi askari wake D.260 P/C.Godlisen anayetuhumiwa kumtumikisha katika vitendo vya ngono mwanafunzi wa kidato cha tatu katika shule ya sekondari Okaoni iliyopo wilaya ya Moshi, mkoani Kilimanjaro.

Mwanafunzi Agripina Andrew CHuwa akiwa amelala kitandani katika wodi namba tano katika Hospital ya Kibosho anakotibiwa majeraha yake baada ya kupata ajali ya pikipiki akiwa na  askari wa kituo cha Polisi Okaoni wakitokea moshi mjini kuelekea Kibosho,anayemuuguza ni mama yake mzazi Modesiana Chuwa.
Habari zilizopatikana hivi karibuni kutoka ndani ya jeshi la polisi mjini hapa zimedai kuwa,askari huo alifikishwa jana kwenye mahakama ya kijeshi ambako pia mwanafunzi huyo aliitwa kutoa ushahidi.

Septemba 21 mwaka huu  askari huyo anatuhumkiwa kumfungia kwenye nyumba ya kulala wageni  iitwayo KUWESE ya mjini hapa ambako anadaiwa kufanya naye mapenzi na baadaye kupata ajali mbaya ya pikipiki na mwanfunzi huyo kupata majeraha kadhaa sehemu mbali mbali za mwili.

Mwanafunzi huyo alikimbizwa katika Hospital ya Rufaa ya KCMC kwa matibabu baada ya kupoteza fahamu lakini alihamishiwa katika Hospital ya Kibosho licha ya hali yake kuendelea kuwa mbaya kwa kile kilichoelezwa ni kukwepa macho ya watu wengi.

Hivi karibuni aliyekuwa akikaimu nafasi ya kamanda wa  polisi mkoa wa Kilimanjaro,Koka Moita  alikiri jeshi la polisi kufungua jarada la chunguzi juu ya tuhuma hizo na kwamba kama itabainika kuwa askari huyo alikwenda kinyume na maadili,hatua za kinidhamu zitachuliwa dhidi yake.

 Kamanda Koka alitetea hatua ya jeshi hilo kutochukua hatua mapema kuhjusiana na tukio hilo akidai kuwa,askari huyo alikuwa akiunguza jeraha alilolipata katika ajili hiyo na kwamba baada ya kupata nafuu aliagiza uchunguzi uanze haraka.

Pamoja na jeshi hilo kumfungulia mashitaka ya kijeshi askari huyo,taarifa kutoka kwa mmoja wa wazazi wa mwanafunzi hiyo zinadai kuwa,kuna juhudi za maksudi zinafanywa na askari wa jeshi hilo kutaka kukwamisha mashitaka hayo ya kijeshi  dhidi ya askari huyo.
Taarifa zinadai kuwa,polisi wa kituo kikuu cha polisi mjini moshi,wanajenga ushawishi kwa wazazi wa mwanafunzi huyo kutaka kulimaliza suala hilo kienyeji huku hali ya mwanafunzi huyo ikielezwa kuwa mbaya kutokana na miguu yake kuvimba.

Akizungumza juu ya mikakati hiyo ya kuharibu mwenendo wa mashitaka,baba mzazi wa mwanafunzi huyo,Andrew Chuwa,alisema  kuwa walishindishwa kutwa nzima nje ya kiuto cha polisi bila kuitwa kwenye mahakama ya kijeshi kutoa ushahidi,huku miguu ya mtoto wake ikiendelea kuvimba kutokana na kushida amesimama katika kituo kikuu cha polisi mjini hapa.

Alidai kuwa,polisi waliita ndungu wa askari anayetuhumiwa kumtumikisha mtoto wake katika vitendo vya ngono wakimshawishi suala hilo walimalize kienyeji  huku akiingiwa na hofu juu ya afya ya mtoto wake.

Mwanafunzi huyo alipelekwa katika Hospital ya mkoa ya Mawenzi kwa ajili ya kufanyiwa vipimo kubaini kama aliingiliwa kimwili na askari huyo na hadi jana majibu ya uchunguzi huo yalikuwa hayajakabidhiwa kwa wazazi wa mwanafunzi huyo.

Naye Diwani wa kata ya Okaoni,ilipo shule hiyo,Morris Makoi,ametishia kuhamasisha na kuitisha maandamano makubwa ya wananchi hadi kituo cha polisi Okaoni kama Jeshi la Polisi litaendelea na danadana juu ya tukio hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari  mjini hapa hivi karibuni,Makoi amesema tukio hilo limewafedhehesha wananchi wengi wa kata ya Okaoni na tarafa nzima ya Kibosho kutokana na kituo hicho kujengwa kwa nguvu za wananchi.

Akamtaka mkuu wa jeshi la polisi nchini(IGP)Ernest Mangu kufumua uongozi wote wa kituo hicho kuanzia mkuu wake wa kituo(OCS) na askari wote na kuleta askari waadilifu na wenye familia.

UVAMIZI MAPITO YA WANYAMA HIFADHI YA TARANGIRE, WATISHIA UHAI WA WANYAMA



H
ifadhi  ya Taifa ya Tarangire ilianzishwa mwaka 1970 kwa tangazo la serikali namba 160 lengo likiwa ni kuhifadhi makimbilio ya wanyama wakati wa majira ya kiangazi.
 
Malengo mengine ya kuanzishwa kwa hifadhi hiyo ni kuhifadhi maeneeo ya mto Tarangire unaobeba jina la hifadhi hiyo pamoja na ardhi oevu ambayo ni chanzo pekee cha maji wakati wa majira ya kiangazi.

Inaaminika kwamba,kipindi hicho cha kiangazi ndicho kipindi ambacho wanyama kunakuwapo na mkusanyiko mkubwa wa wanyama katika eneo la hifadhi.

Wanyama hao  huhama ndnai ya hifadhi hiyo kuelekea masahriki,kaskazini na kusini kwa ajili ya malisho na kuzaliana hususani wanyama kama nyumbu na pundamilia katika miezi ya Oktoba na Novemba ambayo ni kipindi cha masika.

Pamoja na umhimu wa hifadhi hiyo kuichumi kutokana na kuwa moja ya hifadhi tano zinazozalisha ziada,kumekuwapo na changamoto nyingi zinazochanhgia kukwaza shughuli za uhifadhi.

Mkuu wa hifadhi hiyo(CPW),Stephano Qolli,anasema moja ya changamoto zinazokwaza shughuli za uhifadhi ni tishio la kutoweka kwa wanyama kutokana na kuvamiwa kwa mapito yao kutokana na shughuli za kibinadamu.

Anasema kasi ya ongezeko la idadi ya watu na matumizi ya ardhi litaifanya hifadhi hiyo kuwa kisiwa  endapo hatua za makusudi hazitachukuliwa katika kuyalinda mapito hayo ya wanyama.

Katika taarifa yake kwa kamati ya kudumu ya Bunge ya Ardhi,maliasili na mazingira,Mkuu huyo wa hifadhi anasema kuwa,kuna hatari hifadhi hiyo ikatenganishwa na maeneo ya mazalio ya wanyama na mlisho.

Alionya kuwa,wanyama hao wanaweza wakapungua ama kutoweka kabisa endapo maeneo hayo ya malisho yataharibiwa  kutokana na ongezeko kubwa la shughuli za kibinadamu.

Aliwaambia wajumbe wa kamati hiyo kuwa,katika kukabiliana na changamoto hizo,hifadhi imekuwa  ikitoa elimu kwa wananchi na wadau mbalimbali pamoja na kusaidia mradi wa mpango wa mtumizi bora ya ardhi hususani katika vijiji jirani.

Tishio la kuharibiwa vyanzo vya mto Tarangire

Pamoja na tishio la kutoweka  kwa wanyam katika hifahdi hiyo kutokana na kuvamiwa kwa mapito yao,shughuli za kibinadamu ikiwamo kilimo,ufyekaji misitu na ufugaji vimedaiwa kuathiri vyanzo vya maji katika mto tarangire.

Kwa mujibu wa mhifadhi huyo,mto tarangire unaanzia katika milima ya kondoa takribani kilometa 50 kusini mwa hifadhi hiyo ambapo mbali na milima hiyo ya kondoa,pori la akiba la mkungunero nalo ni mojawapo ya chanzo.
Anasema pori hilo pamoja na sehemu ya kusini nalo limevamiwa na mifugo mingi huku shughuli kubwa za kilimo zikiendelea kwa kasi hali ambayo inaweza kuhatarisha uwepo wa hifadhi hiyo.

"tatizo hili linahitaji uelimishwaji wa jamii pamoja na utatuzi wa migogoro ya mipaka kati ya vijiji na maeneo yaliyohifadhiwa na kati ya mikoa ya dodoma na manyara",anasema.


Migogoro ya mipaka

Migogoro ya mipaka ndani ya hifadhi za taifa na misitu ya hifadhi ya taifa limekuwa ni tatizo sugu na ambalo kwa hakika bado halijapatiwa ufumbuzi wa kina na mamlaka husika.

Hali hiyo imeleta misuguano ya mara kwa mara baina ya ungozi wa hifadhi husika kwa upande mmoja na wananchi wanaoishi kuzunguka maeneo hayo ya hifadhi kwa upande wa pili.

Vivyo hivyo hifadhi ya taifa ya tarangire nayo hasijaachwa nyuma katika migogoro hiyo ambko mpaka sasa upo mgogoro unaofukuta katika kijii cha Kimotorok kinachopakana na hifadhi hiyo.

Kijiji hicho kipo wilaya ya Simanjiro lakini mpaka wa kijiji hicho umevuka mpaka wa wilaya na kuingia wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma hivyo utatuzi wake unahitaji ushirikiano wa mikoa hiyo miwili.

Kwa mujibu wa mhifadhi huyo,wananchi wa kijiji hicho hawautambui mpaka wa kijiji kama unavyoonekana katika ramani ya mwaka 1993 huku pia wakikataa kuutambua mpaka wa hifadhi baada ya kuhakikiwa mwaka 204.

Wananchi hao pia wanadaiwa kutolitambua pori la akiba la Mkungunero kwa madai kuwa hawakushirikishwa katika uanzishwaji wake na pia hawautambui mpaka uliopo kati ya mkoa wa Dodoma na Manyara.

Mhifadhi huyo anasema kuwa,endapo eneo hilo   litabaki kwa shughuli za kibinadamu,hifadhi ya tarangire na pori la akiba la Mkungunero zitakuwa
zimetenganishwa.

Anasema kuwa kutenganishwa huko kutaleta athari kubwa kimazingira na kiikolojia ikiwamo kufungwa kwa mapito ya wanyama ambako mapato yatokanayo ya utalii yatapungua.

Ametaja athari nyingine kuwa ni pamoja na uharibifu wa mazingira utakaotokana na kuongezeka kwa shughuli za kibinadamu ikiwamo mifugo,kilimo na makazi hivyo kuathiri mtiririko wa mto Tarangire.

Ngoma ya asili  ikichezwa katika uzinduzi wa mradi wa wa majengo ya vyumba vya madarasa katika shule ya msingi ya Sangaiwe mkoani Manyara uliofanywa na mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge,Ardhi,Maliasili na Mazingira,James Lembeli hivi karibuni

Imetayarishwa na:
Charles Ndagulla
+255-(0)-783 847 877