Alhamisi, 4 Januari 2018

MTOTO WA NDESAMBURO AWAPOZA WALIMU,WAFUNGWA MIAKA MITATU



Na Charles Ndagulla,Moshi

MAHAKAMA ya hakimu mkazi mjini Moshi,imewahukumu kutumikia kifungo cha miaka mitatu jela walimu wawili wa shule ya Msingi ya Mwereni iliyopo wilaya ya Hai baada ya kukutwa na hatia ya kuhamisha umiliki wa shamba la shule isivyo halali.



Hukumu hiyo imetolewa januari 3 mwaka huu na kaimu hakimu mfawidhi  wa mahakama hiyo,Aidan Mwilapwa  baada ya kuwatia hatiani washitakiwa hao .



Walimu waliotiwa hatiani na kuhukumiwa kifungo hicho ni Mwalimu mkuu wa shule hiyo,Onesmo Ernest Kinyaiya na mwalimu mkuu msaidizi wa shule hiyo,Apolinary Denke Pantaleo.

Shamba hilo lilitolewa na walimu hao  kwa mtoto wa Marehemu Philemon Ndesamburo aitwaye Tomm ambaye ni mmoja wa wakurugenzi wa kampuni ya Rahisi General Marchant Ltd ambayo ni kampuni tanzu ya makampuni ya Rahisi Group ya mjini Moshi.



Walimu hao walifikishwa mahakamani hapo na kusomewa mashitaka na waendesha mashitaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(Takukuru),Barry Galinoma akisaidiana na Furahini Kibanga.



Kwa mujibu wa hati ya mashitaka iliyosomwa makahamani hapo na waendesha mashitaka hao wa Takukuru,wlimu hao walishitakiwa kwa kosa la kuhamisha umiliki wa shamba la shule hiyo kwenda kwa kampuni ya Rahisi General Marchant Ltd bila idhini ya kamishna wa Ardhi.



Kulingana na hati hiyo ya mashitaka,walimu hao hawakuwa na mamlaka hayo kwa mujibu wa kifungu cha 17(5) cha sheria ya ardhi ya vijijini sura ya 14 kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2002.



Hivyo  uhamishaji huo ulikuwa kinyume na kifungu cha 31 cha sheria ya Kuzuia na Kupambana na rushwa namba 11 ya mwaka 2007 hivyo mahakama hiyo kuwatia hatiani katika shauri hilo la jinai namba 3 la mwaka 2016.



Katika hukumu hiyo,walimu hao walihukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela au faini ya shilingi laki tano na baada ya mahakama kuwatia hatiani walimu hao walinusurika kwenda jela baada ya ndugu walikuwa wamefurika mahakanai hapo kuchangishana fedha na kuwalipia faini.



Baada ya hukumu hiyo,Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa(Takukuru) mkoani Kilimanjaro,imetoa taarifa kupitia kwa Mkuu wa Taasisi hiyo mkoani hapa,Holle Makungu kuwa itafuatilia kwa mwajiri wa walimu hao ili kuhakikisha wanaondolewa kwenye utumishi wa umma.





KARANI MAHAKAMA YA MWANZO  MBARONI KWA RUSHWA YA LAKI MOJA.



Katika tukio jingine,mtego ulioandaliwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(Takukuru),umefanikiwa kumnasa karani mmoja wa mahakama ya Mwanzo iliyopo Maili Sita wilaya ya Hai .



Karani huyo,Rose Jonathan Urassa(58),alinaswa na Takukuru baada ya kudai rushwa ya shilingi laki moja ili amsaidie mshitakiwa katika shauri la jinai namba 69/2017 kupitia kwa hakimu anayesikiliza shauri hilo.



Taarifa ya Takukuru mkoani Kilimanjaro iliyotolewa kwa vyombo vya habari leo Januari 4 na kusainiwa na Mkuu wa Takukuru mkoa(RBC),Holle Makungu imeeleza kuwa,karani huyo aliomba fedha hizo ili hakimu anayesikiliza shauri hilo aweze kutoa hukumu ya upendeleo kwa mshitakiwa.



“Baada ya taarifa hizo kupokelewa,mtego wa rushwa uliandaliwa na aliweza kukamatwa januari 3 mwaka huu akiwa amepokea fedha hizo katika eneo hilo  la mahakama ya mwanzo,Hai,Rose atafikishwa mahakamani mara uchunguzi utakapokamilika”,imesema taarifa hiyo.



Takukuru imetoa  onyo kwa baadhi ya makarani na wahudumu wa mahakama wanaoendekeza tabia ya kuomba na kupokea rushwa kwa kisingizio cha kutumwa na waheshimiwa mahakimu wabadili tabia hiyo.



Kamanda Makungu katika taarifa yake hiyo kwa vyombo vya habari,ametoa rai kwa makarani na wahudumu wa mahakama katika mkoa wa Kilimanjaro wanaoendelea  na tabia hiyo mwisho wao wa  kufanyakazi katika utumishi wa umma kwa mwaka huu 2018 utakuwa mwisho wao.



Pia alitoa wito kwa wananchi wanaodaiwa rushwa na baadhi ya makarani na wahudumu wa mahakama kwa kisingizio cha  kutumwa na waheshimiwa mahakimu,watoe taarifa kwa taasisi hiyo ili iweze kuboresha mahakama kwa kuwaondoa wachache wanochafua sura za mahakama.


Maoni 1 :

  1. SAFARI YAKO YA MAFANIKIO UTAJIRI NA RIZIKI ZAKO ZIMESIMAMA NA KUZINASUA UWEZE KUSONGA MBELE SOMA KWA UMAKINI UWEZE KUIJUA SIRI HII.

    KATIKA SAFARI YA MAFANIKIO TUNAPITIA MENGI ILI TUWEZE KUFANIKIWA LAKINI WENGI WETU KUNA MAMBO MACHACHE SANA WENGI WETU TUNAYADHARAU NA KUMBE NDIO CHANZO CHA MAFNIKIO YETU.

    N.B KWA WALE WAHITAJI WA PESA ZA NDAGU au MAJINI kwa mudamfupi nipigie DOKTA MDIRO +255 742162843
    MALIPO NI BAADA YA KUFANIKIWA PIA UMBALI POPOTE ULIPO KENYA,UGANDA, OMAN, CONGO RWANDA N.K
    WOTE NAWAKARIBISHA.

    (kuhusu utajiri au pesa) KABLA YA KUPIGA SIMU ZINGATIA YAFUATAYO
    1. uwe una umri wa miaka 18+
    2. uwe tayari kupokea masharti yote
    3.uwe na uwezo wa kutunza siri
    4. uwe jasiri wa kupokea taarifa yoyote
    KARIBU SANA KWA SHIDA NYINGINE PIA ULIYONAYO AMBAYO SIJATAJA INSHAALAH ITATATULIWA IKIWA NDANI YA UWEZO WANGU.(HUSITUME SMS PIGA SIMU KUHEPUKA MATAPELI)

    HAYA NI MAMBO 7 YAKUZINGATIA KATIKA SAFARI YAKO YA MAFNIKIO

    i) Wazazi wako wakiwa wamekulea mpaka ukawa mkubwa wafumbua macho unawaona akikisha usiwafanye wakajuta kukuzaa asilimia kubwa wazazi wanakuwa na tabu sana ila zile tabu zao ndio zinazokufanya wewe una aminiwa na watu na unaeshimika na kujieshimu

    Kwaiyo jitahidi sana kuwa nao vizuri kuna wengi maisha yao wanaishi kwa shida chanzo ni utofauti baina ya wazazi wao

    Ukiona wazazi wako wanatabu sana usiwajibu vibaya wewe kaa nao mbali ila wape majukumu yao unacho fanya kuwaona nakurudi ulipo apo utaona mambo yako yatakuwa vizuri sana

    ii) JAMBO LA PILI
    Akikisha unatunza uzao wako yani ukijua ni mtoto ni wako basi jitahidi sana kutoa uduma ata kidogo ulicho nacho lakini udumia usiache uzao wako unateseka na njaa wewe una kula maisha aisee fahau

    Kila mtoto wako anavyo kuwa ndio mambo yako yanaaribika usipo udumia kwaiyo ukiwa waitaji kufanikiwa zaidi jali uzao wako

    iii) JAMBO LA TATU
    ukiwa umeoa au umeolewa usitoe talaka au kuomba talaka kabla mwenzio ayupo tayari kwa muda huo fahamu ukiomba talaka au akikupa talaka bila bila sababu ya msingi yeye tu ana matamanio ya kidunia basi anamuda atapoteza muelekeo wa maisha yake

    iv) UKIWA WAPATA PESA
    ukiwa wapata pesa alafu utoi sadaka basi kufikia kwenye ukuu utachelewa sana mana mana pesa badala ya kutoa kwa iyari yako utatoa kwa matatizo kwaiyo jitahidi icho icho kidogo toa sadaka kwa wenye uitaji

    v) USIMZULUMU MTU
    kama wataka kufika mbali kwenye mafanikio yako usimzulumu mtu ata kwa uchache wa kitu usifanye ivyo itakugarimu kiasi kikubwa

    vi) USIZARAH MILA
    ukiwa kwenu kuna mambo ya mila mzimu tambiko jitahidi kufatilia sana aya mambo yanarudisha nyuma sana usipo yawahi mapema

    vii)USIWE WA NAMNA
    1)ikiwa ujafanikiwa jitahidi sana usiwe mvivu kufanya kazi usiwe muhuni usiwe mwenye chuki na asira zisizo za msingi usiwe na tamaa nyoa vizuri vaa nguo za eshima na usiige maisha ya watu.

    KWA MAWSILIANO ZAIDI KUHUSU MATATIZO MBALIMBALI YA TIBA ASILI NA TIBA MBADALA, PETE MALI ZA NDAGU NA MAJINI N.K

    DOKTA MDIRO Call/whatsup +255 742162843.

    JibuFuta