Jumatano, 26 Novemba 2014

KADI 'HARAMU' ZAIVURUGA CCM, MWANGA



Hali  ya kisiasa ndani ya Chama Cha Mapinduzi(CCM) wilayani Mwanga si shwari kutokana na kuibuka kwa kundi linalotoa kadi za chama hichokwa wanachama wapya bila utaratibu kwa misingi ya kujijenga kisiasa kuelekea uchaguzi mkuu ujao na chaguzi za viongozi wa serikali za mitaa,vijiji na vitongoji mapema mwezi ujao.

Habari zilizopatikana hivi karibuni kutoka wilayani mwanga na kudhibitishwa na mbunge wa jimbo hilo,Profesa Jumanne Maghembe,zinadai kuwa tayari kadi haramu 3,000 zimeingizwa wilayani humo na kugawanywa kwa wanachama wapaya bila kufuata tararibu za kichama.

Akizungumza kutoka bungeni  mjini Dodoma, Maghembe amedai kuwa, wanaosambaza kadi hizo bado zinasambazwa kama njugu katika maeneo kadhaa ya jimbo hilo na kukitaka chama hicho kuchukua hatua kwa wanaoendesha mchezo huo mchafu .

Kadi zinatolewa kwa wingi katika maeneo ya Kighare,Kilomeni,Kirongwe ambako taarifa zinadai kuwa zinatolewa bila utaratibu ikiwamo wanachama kupewa bila kuomba na kutojadiliwa kwenye matawi .

Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Kilimanjaro,Juma Idd alisema kuwa tayari wameagiza uchunguzi kufanyika na kubaini kama kadi hizo zinatolewa nje ya utaratibu na kwamba watakaobainika kufanya hivyo watawajibishwa kwa mujibu wa taratibu.

Hata hivyo mwenyekiti huyo alikwepa kuweka wazi juu ya mpasuko uliopo ndani ya kamati ya siasa ya wilaya hiyo ambako taarifa zinadai kuwa baadhi ya wajumbe wake hawasalimiani hali ambayo inaelezwa kuibua makundi mawili .

Kundi moja ndani ya kamati hiyo ya siasa ni lile linalomuunga mkono mbunge wa sasa Profesa Jumanne Maghembe na jingine likimuunga mkono MNEC,Joseph Thadayo ambaye katika uchaguzi mkuu mwaka 2010,alibwagwa na Maghembe kwenye kura za maoni.

Kutokana na mpasuko huo,baadhi ya wanaccm  waliozungumza na blog wamekitaka chama hicho makao makuu kuunda tume ya kuchunguza sakata hilo  kwa kile walichodai kuwa kamati ya siasa ya wilaya imeparanganyika.

Wamedai kuwa,kamati hiyo haiwezi kutoa matokeo mazuri ya uchunguzi kutokana na mparanganyiko huo kwani hadi sasa wajumbe wa kamati hiyo hawashirikiani hata katika shughuli za maendeleo hata kufikia hatua ya kutozikana.

Mmoja wa wajumbe wa kamati hiyo,ndiye anayedaiwa kufadhili mpango huo wa kusambaza kadi harahamu kwa lengo la kupanua wingo wa kisiasa na kujiongezea wajumbe wengi wenye ushawishi mkubwa katika zoezi la upigaji wa kura za maoni.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni