Jumamosi, 11 Novemba 2017

UELEKEO MPYA MALIASILI NA UTALII- DKT.HAMISI KIGWANGALLA



KWA UFUPI: Uelekeo Mpya wa Maliasili na Utalii.
-------------------
Na Dkt. Hamisi Kigwangalla.


Tunajipanga kufanya makubwa yafuatayo:
Moja, kuongeza idadi ya wageni kuingia nchini kwa kufanya 'offensive marketing'. 

Tunaweka mikakati ya kuvutia zaidi watalii kutoka masoko mapya ya middle east (kipindi chao cha joto kali) na Far East (Tunaunda package maalum za kanda hizi).

Tutakuza idadi ya watalii wa ndani kwa kutumia mikakati mseto ya kutangaza utalii wa ndani na tunatengeneza 'package' rahisi ya watalii wa ndani kwa ajili ya kuvutia watalii wa ndani hususan kwenye vipindi vya 'low season'.

Pamoja na 'packaging strategy' yetu kulenga masoko fulani maalum, tunalenga kuitangaza zaidi nchi yetu kwenye 'travel expos' nyingi zaidi duniani (wiki hii nimetuma team yetu kwenye maonesho ya safari makubwa zaidi duniani yanayojulikana kama 'World Travel Market'.

Na wameambatana na Tour Operators kadhaa ambao watafanya mikutano ya 'networking' na wenzao wa masoko mengine duniani.

Pia tunalenga kutumia role models na hususan travel bloggers mashuhuri duniani kuja kutalii na kushuhudia vivutio vyetu kisha kuweka 'experience' zao kwa picha ama video kwenye 'social media accounts' zao.

We need more presence kwenye social networks ili kuvionesha vivutio vyetu na tutapenya kwenye masoko hayo niliyoyataja kwa kutumia watu mashuhuri wanaopatikana kwenye makundi haya ya masoko niliyoyataja.

Tutaendelea kuyalinda masoko yetu 'traditional' ya nchi za Ulaya na Marekani ya Kaskazini (defensive strategy) kwa mikakati hiyo hiyo.

Mbili, tunawekeza zaidi nguvu zetu kwenye kuongeza idadi ya siku ambazo watalii wanakaa nchini kwa kuongeza idadi ya vivutio na shughuli ambazo mtalii atafanya hapa nchini.

Tutawekeza nguvu zetu kwenye kuanzisha vivutio vya burudani na vya utamaduni. Tuko mbioni kuanzisha Dar Bus Tour, Arusha Bus Tour, Presidential Museum, Theme Park, Tanzania Heritage Month.

Tatu, tunaendelea kuhifadhi vivutio vyetu vya kipekee vya wanyamapori, uoto wa asili, mito, milima na fukwe, malikale na kuwekeza kwenye 'information centers' kwenye vivutio hivi. Pia kualika wawekezaji kujenga facilities kwa ajili ya wageni kwenye vivutio vipya na maeneo mapya ya kitalii.

Nne, tutawekeza kwa kushirikiana na taasisi nyingine, za umma na binafsi, kwenye utalii wa mikutano na Utalii wa matukio (michezo, mashindano nk). Malengo yakiwa ni kuvutia zaidi matukio ya kikanda na kimataifa kufanyikia nchini mwetu.

Tano, mambo mtambuka ya kimkakati tunayofanya ni pamoja na kwenda 'electronic' kwenye ukusanyaji mapato, huduma kwa watalii na usalama wa wanyamapori, usalama wa maeneo ya vivutio na usalama wa watalii wetu.

Kuunganisha uchumi wa watu wanaotuzunguka na shughuli za uhifadhi na Utalii kwa ujumla wake, na kuimarisha mnyororo mzima wa huduma za ukarimu nchini.

Mwisho, nimeagiza taasisi zote chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii kuwekeza kwenye mkakati huu wa 'diversification' ya vivutio na kuongeza idadi ya siku na kiasi cha fedha ambazo mtalii anatumia nchini kwetu.

 Aidha, vivutio vipya lazima viunganishwe na sakiti za sasa na mpya za utalii tunazozungumzia. Na ni lazima viwahusishe wananchi wa maeneo husika (linkage ya utalii na maisha ya wananchi).

Ijumaa, 10 Novemba 2017

MKAKATI WA KUZALISHA KAHAWA UMEKWAMA



Na Charles Ndagulla,Moshi

MWAKA 2011,serikali kuu kupitia  bodi ya kahawa nchini(TCB) iliweka mkakati wa miaka 10 wa kuendeleza tasnia ya kahawa(Coffe Industry  Development Strategy,2011-2021) kwa lengo la kuendeleza kilimo cha zao hilo nchini kwa kushirikiana na wadau mbali mbali katika sekta hiyo.

Lengo la mkakati huo ilikuwa ni  kuongeza uzalishaji,tija na ubora wa kahawa na kuboresha mapato katika mnyororo wote wa thamani hususani wakulima wa kahawa  na  kuwezesha kahawa ya Tanzania kupata bei nzuri kwenye soko la dunia.

Hata hivyo mkakati huo umekwama kutokana na changamoto kadha za uzalishaji ikiwamo tija ndogo ya uzalishaji inayochangiwa na matumizi kidogo ya pembejeo hususani mbolea .

Mkakati huo ulilenga kuongeza uzalishaji wa kahawa safi kwa mwaka  kutoka tani 50,000  hadi kufikia tani laki moja ifikapo mwaka 2021 lakini hadi kufikia msimu wa 2016/2017 uzalishaji wa kahawa ulikuwa tani 46,963.5.

Sababu nyingine zilizokwaza mkakati huo zinatajwa kuwa ni kasi ndogo ya kupokea matokoeo ya utafiti,mabadiliko ya tabianchi yanayaodaiwa kusababisha mvua zisizo na mpangilio pamoja na uwekezaji mdogo ikilinganishwa na malengo ya mkakati huo.

Uchunguzi wa jamhuri umebaini kuwa,katika misimu saba iliyopita uzalishaji wa zao la kahawa nchini umekuwa ukipanda na kushuka huku baadhi ya wakulima wakidaiwa kulipa kisogo zao hilo na kugeukia mazao mseto kutokana na kupanda kwa gharama za uzalishaji na bei ndogo.

Katika msimu wa 2010/2011 uzalishaji wa kahawa ulikuwa tani 56,790.0 lakini msimu uliofuata wa 2011/2012 uzalishaji ulishuka kwa kasi ya kutisha na kufikia tani 33,086.7 na ulipanda tena msimu wa 2012/2013 na kufikia tani 71,319.1.

Msimu wa 2013/2014 tani 48,761.9 zilizalishwa na tani hizo zilishuka tena msimu wa 2014/2015 na kufikia 42,768.0 na kupanda tena katika msimu wa 2015/2016 hadi tani 60,188.0 kabla ya kuporomoka msimu wa 2016/2017 hadi tani 46,963.0.


Kaimu mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya kahawa nchini(TCB),Primus Kimaryo anasema utazalishaji wa kahawa katika msimu wa 2017/2018 unatarajiwa kushuka kutoka tani 46,963.0 hadi kufikia tani 43,000.

Jumatano, 4 Februari 2015

RAIS GAUCK KATIKA SIKU YA PILI YA ZIARA, TANZANIA



Rais wa Ujerumani, Joachim Gauck, anaendelea na ziara yake nchini Tanzania, ambapo leo atatembelea visiwani Zanzibar, na kufanya mazungumzo na Rais Ali Mohamed Shein. 

Katika kukamilisha siku ya kwanza ya ziara hiyo jana usiku, Rais Gauck alikula chakula cha jioni alichoandaliwa na mwenyeji wake Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika Ikulu ya Dar es Salaam. 

Gauck ameyasifu maendeleo ya kisiasa na kiuchumi ya Tanzania, ingawa amesema bado mengi yanapaswa kufanyika ili kuwawezesha wananchi wa kawaida. 

Amerejelea mtazamo wa Ujerumani kwa Tanzania kama taifa la Afrika Mashariki linaloinukia kwa kasi kiuchumi, hatua ambayo amesema inachangiwa na uwepo wa amani na utulivu wa kisiasa. 

Aidha, Rais Kikwete ameitaka Ujerumani kuimarisha uwekezaji wake kwenye sekta kadhaa zinazokuwa nchini Tanzania, hasa katika soko la utalii ambalo tayari Ujerumani imeonyesha muelekeo mzuri. 

Ziara hiyo itamfikisha Gauck hadi mkoani Arusha.

Jumanne, 3 Februari 2015

AWEKEWA MIKONO YA MTU MWINGINE, INDIA



Madaktari katika Chuo cha Tiba cha Amrita, Kochi huko India wamefanikiwa kufanya upasuaji wa aina yake wa kupandikiza mikono mipya kwa binadamu aliyekatika viungo hivyo.

Upandikizaji huo uliofanyika Januari 12 na 13, ulifanikiwa kwa mara ya kwanza, baada mwanamume mwenye umri wa miaka 30, aliyekatika mikono katika ajali ya treni kuwekewa mingine. Mikono hiyo mipya ilichukuliwa kutoka kwa kijana wa miaka 24 aliyepata aliyefariki katika ajali ya gari.

Mkuu wa kitengo cha upasuaji katika chuo hicho, Profesa Subramania Iyer alisema: “Siku 14 baada ya upasuaji, mikono ilikubaliwa na mwili na ikaanza kujongea, yaani aliyepandikizwa aliweza kuisogeza huku na kule. Mgonjwa alitolewa chumba cha wagonjwa mahututi na huduma nyingine za kumchunguza ziliendelea.”

Daktari katika Taasisi ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu Hospitali ya Muhimbili (Moi), Profesa John Kahamba alisema hiyo si mara ya kwanza kwa upandikizaji wa mikono kufanyika duniani kwani na tofauti kubwa na upandikizaji wa figo au ini.

MIAKA 38 YA CHAMA CHA MAPINDUZI YAFANYIKA SONGEA



Mwenyekiti wa CCM Taifa ,Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akivishwa skafu na kijana wa chipukizi mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa Maji Maji mjini Songea kwenye sherehe za  maadhimisho ya miaka 38 ya kuzaliwa kwa  CCM.



Jumapili, 1 Februari 2015

DOLA LA KIISLAMU LAUA MWANDISHI WA HABARI



Wanamgambo wa itikadi kali wa dola ya kiislam-IS wadhihirika wamemuuwa  pia habusi wa pili wa Japan.Wamechapisha kanda ya video kupitia mtandao wa internet,inayoonyesha mwandishi habari Kenji Goto amekatwa kichwa.

Waziri wa ulinzi wa Japan Gen Nakatani amesema kanda hiyo ya video inaonyesha ni ya kweli.Katika kanda hiyo ya video anaonekana mtu aliyeficha uso wake akimuonya waziri mkuu wa Japan Shinzo Abe "jinamizi limeshanza kuikaba Japan." 

Serikali mjini Tokyo ilitangaza kati kati ya mwezi uliopita wa january kutenga  dala milioni 200 kama msaada ambao si wa kijeshi kwaajili ya mapambano dhidi ya wanamgambo wa IS.Waziri mkuu Abe ameshasema hawatoupigia magoti ugaidi.

Rais Barack Obama wa Marekani amelaani kitendo hicho kuwa ni cha kinyama.Katibu mkuu wa Umoja wa mataifa Ban Ki-Moon amelaani "mauwaji ya kishenzi" ya Goto na kuwataka wafuasi hao wa itikadi kali wawaachie huru haraka mahabusi wote wanaowashikilia.Jordan pia imelaani vikali kuuliwa mwandishi habari wa pili wa Japan Kenji Goto.
CHANZO: DW