Ijumaa, 16 Machi 2018

MTUMISHI PPF ALIYENASWA NA DAWA ZA KULEVYA AENDELEA KUSOTA GEREZANI

  MTUMISHI  wa mfuko wa Pensheni kwa watumishi wa umma(PPF)mkoani    Kilimanjaro   ,Anitha Osward(32)anayetuhumiwa kusafrisha shehena ya dawa za kulevya,ameendelea kusota gerezani katika gereza Kuu la Mkoa wa Kilimanjaro,Karanga baada ya gari la mahabusu kuharibika.

Anitha Mkazi wa Karanga Manispaa ya Moshi,alikamatwa desemba 19 mwaka jana akiwa na shehena ya madawa ya kulevya aina ya mirungi aliyokuwa akiisafrisha kwa kutumia gari lake dogo aina ya Toyota Sienta lenye namba za usajili T674DLB.

Alikamatwa na askari wa Doria eneo la Majengo kwa Mtei mjini Moshi akiwa  anasafirisha dawa za kulevya aina ya mirungi kilo 216 na gramu 370”. 
Kutokana na kuharibika kwa karandinga la polisi,kesi hiyo sasa imepigwa kalenda hadi machi 27 mwaka huu itakapokuja kwa ajili ya kutajwa katika mahakama ya hakimu mkazi mjini Moshi kutokana na upelelezi wa shauri lake kutokamilika.

Katika kesi hiyo,dereva taksi mkazi wa mjini moshi,Frank Sifael Moshi maarufu kwa jina la ‘Gaucho’ameunganishwa na Anitha na inadaiwa ndiye aliyekuwa akiendesha gari la Anitha wakati wa tukio hilo.
Hata hivyo dereva huyo alitimua mbio baada ya gari hilo kusimamishwa na polisi wa doria na kumwacha Anitha akiangukia mikononi mwa polisi jaoo naye arobaini yake ilitimia baada ya kunaswa na polisi.
 Anitha Osward,mtuhumiwa wa dawa za kulevya,akiwa mikononi mwa polisi muda mfupi baada ya kukamatwa akituhumiwa kusafrisha shehena ya dawa za kulevya aina ya Morungi.
 Hii ndiyo shehena ya dawa za kulevya aina ya mirungi ambayo ilikamatwa ndani ya Gari la Anitha Osward lenye namba za usajili T674DLB aina ya Toyota Sienta,tayari Anitha na dereva wake Frank Sifael Moshi a.k.a Gaucho,wameshafikishwa makahamani wakishitakiwa kwa kosa la kusafrisha dawa za kulevya.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni