Jumamosi, 17 Machi 2018

WASIOLIPA ANKARA ZA MAJI MUWSA WAKIONA CHA MOTO,POLISI,MAGEREZA WAVUTIWA PUMZI


NA KIJA ELIAS, MOSHI. 

Mamlaka ya maji safi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi (MUWSA), imewasitishia huduma ya maji safi na salama wakazi zaidi ya 1,503,  kutokana na kushindwa kulipa malimbikkizo ya ankara za maji wanayodaiwa na Mamlaka hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habati hivi karibuni,Mkurugenzi wa Mamalaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi Joyce Msiru alisema kuwa wateja hao wanadaiwa zaidi ya shilingi Milioni 143.7.

Alikuwa akizungumza kuelekea maadhimisho ya wiki ya maji ambayo huadhimishwa kila mwaka nchini kote kuanzia machi 16 hadi 22  ambako alitumia muda huo kuwaasa wateja wenye madeni kulipa ankara zao ili kukwepa adha ya kusitishiwa huduma hiyo mhimu .

Alisema katika kuadhimishi wiki ya maji mjini hapa Mamlaka hiyo inakusudia kufanya promosheni   mbali mbali kwa wateja wake watakaounganishiwa huduma ya maji safi na maji taka  wakiwemo waliositishiwa huduma ya maji kutokana na malimbikizo ya ankara za maji.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji safi na uondoshaji wa maji taka Moshi Mjini(MUWSA),Joyce Msiru akipanda mti ikiwa ni uzinduzi wa wiki ya maji inayoadhimishwa kila mwaka kuanzia machi 16 hadi 22.

“Tutakuwa na wiki ya maji, wateja wa maji safi ambao watalipa madeni yao katika wiki ya maji watasamehewa faini ya shilingi 20,000 za kurudishiwa huduma ya maji majumbani mwao na kwa wale watakaohitaji kuunganishiwa huduma ya maji taka watalazimika kulipia nusu ya gharama zinazohitaji na sehemu iliyobaki wataendelea kulipa kwa awamu,”alisema.

Akizungumzia wiki ya maji Mkurugenzi huyo alisema itakwenda pamoja na zoezi la usafi wa mazingira katika soko la Manyema mjini hapa,kuwa na maonyesho ya shughuli mbali mbali zinazofanywa na Muwsa ikiwemo utoaji wa elimu kwa watumiaji wa maji na kuendesha zoezi la upandaji wa miti zaidi ya 12,000 katika vyanzo mbali mbali vya maji mjini hapa.

Meneja biashara wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira John Ndetico, alisema Mamlaka hiyo inakusudia kuzikatia huduma ya kupata maji safi  taasisi za serikali ikiwemo Ofisi ya Kamanda wa Polisi mkoani hapa (RPC)Jeshi la magereza  na shule ya mafunzo ya awali ya polisi (CCP) iliyopo mjini hapa.
 Mkuu wa wilaya ya Moshi,Kippi Warioba akipanda mti kuashiria uzinduzi wa wiki ya maji mjini Moshi

Alisema licha ya serikali kuahidi kuzilipitia taasisi hizo madeni hayo bado zinaendelea kulimbikiza madeni yao na kwamba Muwsa tayari imeshaziandikia baraua za kuziarifu kuzisitishia huduma ya kupata maji safi.

‘Taasisi hizo zilikuwa zinadaiwa malimbikizo ya zaidi ya shilingi 320 milioni lakini madeni hayo yameongezeka hadi kufikia Julai 2017 bilioni 1.8 na kwamba taasisi hizo hazionyeshi nia ya kulipa malimbikizo hayo licha ya serikali kuahidi kuzilipia madeni yao yanayoishia june 2017 ambapo kupitia hazina madai hayo yapo kwenye zoezi la uhakiki ili yaweze kulipwa”alisema Ndetiko.
 Mkuu wa wilaya ya Moshi,Kippi Warioba(wa pili kutoka kulia) akikatra utepe kuzindua mfumo wa malipo ya huduma za majisafi na majitaka kupitia NMB Mobile ikiwa ni sehemu  ya maadhimisho ya wiki ya maji.
 TUNATEKELEZA: pichani ni Florah Nguma,kaimu ofisa uhusiano MUWSA akipanda mti katika uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya maji ambayo uliofanyika mjini moshi

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni