Jumamosi, 30 Desemba 2017

UJENZI WA NYUMBA SASA KWA KIBALI,WATAKAOPUUZA KUKIONA



Na Kija Elias, Hai.

Baraza la Madiwani la halmashauri ya wilaya ya Hai, mkoani Kilimanjaro, limepitisha sheria ndogo ndogo zikiwemo sheria za vibali vya ujenzi vinayomtaka kila mwananchi ambaye anataka kujenga lazima awe na kibali cha ujenzi huo. 

Sheria hiyo imepitishwa jana, kufuatia agizo lililotolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi ambalo alilitoa hivi karibuni la kuwataka viongozi wa Halmashauri za wilaya,miji Majiji nchini, kuharakisha utoaji wa vibali vya ujenzi na kuachana na urasimu ambao ulikuwa ukisababisha kuwepo kwa ujenzi holela. 

Akisoma sheria hizo kwa niaba ya Mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Afisa Ardhi wa wilaya hiyo Jacob Muhumba, alisema kuwa mtu yeyote atakaye jenga bila kuwa na kibali cha ujenzi sheria hiyo imeweka adhabu kali ikiwa ni pamoja na kusitisha ujenzi wake na kufikishwa katika vyombo vya dola. 

“Sheria hii inamtaka kila mtu anayetaka kujenga ni lazima awe na kibali cha ujenzi, hatutamruhusu mtu kujenga bila kuwa na kibali, na kila mtu atakayekuwa anaomba kibali cha ujenzi atalazimika kulipia gharama  kwa ajili ya kupata kibali hicho,”alisema Muhumba. 

“Tulikuwa hatuna sheria ya vibali vya ujenzi tangu zamani, lakini pia tulikuwa hatutozi gharama yeyote ile, hivyo mwananchi alikuwa akijijengea tu bila kufuata utaratibu hali ambayo imechangia kuwepo kwa makazi holela,”alisema. 

Aidha alifafanua kuwa gharama hizo za kupata kibali cha ujenzi kitategemea na kile mtu anachotaka kujenga , ikiwemo ujenzi wa nyumba za makazi, maghala, viwanja vya ndege na majengo ya biashara . 

Kwa upande wake Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya hiyo, Helgha Mchomvu alisema kuwa baraza hilo limelazimika kuipitisha  sheria hiyo ili kuepusha ujenzi holela ambao umekuwa ukifanyika na hivyo kuufanya mji wa Bomang’omba kutokuwa katika mpangilio mzuri. 

Katika hatua nyingine halmashauri hiyo ya wilaya ya Hai,imeshindwa kufikia lengo la kukusanya mapato ya shilingi Bilioni 2.5 kutokana na baadhi ya vyanzo vya mapato vya halmashauri hiyo kuchukuliwa na serikali Kuu.
  

“Ukusanyaji wa mapato umeshuka kutoka bilioni 2.5 hadi kufikia bilioni 2.1 hii imechangiwa na serikali kuu kuchukua vyanzo vyetu ambavyo tulikuwa tukikusanya, hivyo kupitishwa kwa sheria ya kuwa na kibali cha ujenzi itasaidia kuongeza ukusanyaji wa mapato,”alisema mwenyekiti wa halmashauri hiyo.

Wakizungumzia hatua ya kuwepo na sheria ya vibali katika ujenzi wa nyumba baadhi ya wakazi wa  mji wa Boma ng’ombe, kuhusu  wamesema kuwa itasaidia sana kwani kumekuwepo na ujenzi holela ambao unachangia kuharibu mandhari ya mji huo.

Gidion Lucas na Issaya Fabiani, walisema kumekuwepo na ucheleweshaji mkubwa wa kupata vibali vya ujenzi unaosababishwa na wahusika wenyewe na hivyo kuchangia wananchi kujenga kiholela bila kufuata utaratibu, kutokana na kuchoka kusubiri  kwa muda mrefu ili waweze kupata vibali vya ujenzi.



Maoni 1 :

  1. SAFARI YAKO YA MAFANIKIO UTAJIRI NA RIZIKI ZAKO ZIMESIMAMA NA KUZINASUA UWEZE KUSONGA MBELE SOMA KWA UMAKINI UWEZE KUIJUA SIRI HII.

    KATIKA SAFARI YA MAFANIKIO TUNAPITIA MENGI ILI TUWEZE KUFANIKIWA LAKINI WENGI WETU KUNA MAMBO MACHACHE SANA WENGI WETU TUNAYADHARAU NA KUMBE NDIO CHANZO CHA MAFNIKIO YETU.

    N.B KWA WALE WAHITAJI WA PESA ZA NDAGU au MAJINI kwa mudamfupi nipigie DOKTA MDIRO +255 742162843
    MALIPO NI BAADA YA KUFANIKIWA PIA UMBALI POPOTE ULIPO KENYA,UGANDA, OMAN, CONGO RWANDA N.K
    WOTE NAWAKARIBISHA.

    (kuhusu utajiri au pesa) KABLA YA KUPIGA SIMU ZINGATIA YAFUATAYO
    1. uwe una umri wa miaka 18+
    2. uwe tayari kupokea masharti yote
    3.uwe na uwezo wa kutunza siri
    4. uwe jasiri wa kupokea taarifa yoyote
    KARIBU SANA KWA SHIDA NYINGINE PIA ULIYONAYO AMBAYO SIJATAJA INSHAALAH ITATATULIWA IKIWA NDANI YA UWEZO WANGU.(HUSITUME SMS PIGA SIMU KUHEPUKA MATAPELI)

    HAYA NI MAMBO 7 YAKUZINGATIA KATIKA SAFARI YAKO YA MAFNIKIO

    i) Wazazi wako wakiwa wamekulea mpaka ukawa mkubwa wafumbua macho unawaona akikisha usiwafanye wakajuta kukuzaa asilimia kubwa wazazi wanakuwa na tabu sana ila zile tabu zao ndio zinazokufanya wewe una aminiwa na watu na unaeshimika na kujieshimu

    Kwaiyo jitahidi sana kuwa nao vizuri kuna wengi maisha yao wanaishi kwa shida chanzo ni utofauti baina ya wazazi wao

    Ukiona wazazi wako wanatabu sana usiwajibu vibaya wewe kaa nao mbali ila wape majukumu yao unacho fanya kuwaona nakurudi ulipo apo utaona mambo yako yatakuwa vizuri sana

    ii) JAMBO LA PILI
    Akikisha unatunza uzao wako yani ukijua ni mtoto ni wako basi jitahidi sana kutoa uduma ata kidogo ulicho nacho lakini udumia usiache uzao wako unateseka na njaa wewe una kula maisha aisee fahau

    Kila mtoto wako anavyo kuwa ndio mambo yako yanaaribika usipo udumia kwaiyo ukiwa waitaji kufanikiwa zaidi jali uzao wako

    iii) JAMBO LA TATU
    ukiwa umeoa au umeolewa usitoe talaka au kuomba talaka kabla mwenzio ayupo tayari kwa muda huo fahamu ukiomba talaka au akikupa talaka bila bila sababu ya msingi yeye tu ana matamanio ya kidunia basi anamuda atapoteza muelekeo wa maisha yake

    iv) UKIWA WAPATA PESA
    ukiwa wapata pesa alafu utoi sadaka basi kufikia kwenye ukuu utachelewa sana mana mana pesa badala ya kutoa kwa iyari yako utatoa kwa matatizo kwaiyo jitahidi icho icho kidogo toa sadaka kwa wenye uitaji

    v) USIMZULUMU MTU
    kama wataka kufika mbali kwenye mafanikio yako usimzulumu mtu ata kwa uchache wa kitu usifanye ivyo itakugarimu kiasi kikubwa

    vi) USIZARAH MILA
    ukiwa kwenu kuna mambo ya mila mzimu tambiko jitahidi kufatilia sana aya mambo yanarudisha nyuma sana usipo yawahi mapema

    vii)USIWE WA NAMNA
    1)ikiwa ujafanikiwa jitahidi sana usiwe mvivu kufanya kazi usiwe muhuni usiwe mwenye chuki na asira zisizo za msingi usiwe na tamaa nyoa vizuri vaa nguo za eshima na usiige maisha ya watu.

    KWA MAWSILIANO ZAIDI KUHUSU MATATIZO MBALIMBALI YA TIBA ASILI NA TIBA MBADALA, PETE MALI ZA NDAGU NA MAJINI N.K

    DOKTA MDIRO Call/whatsup +255 742162843.

    JibuFuta