Jumamosi, 23 Desemba 2017

BREAKING NEWS:MTUMISHI WA SHIRIKA LA UMMA AKAMATWA NA SHEHENA YA DAWA ZA KULEVYA



JESHI la polisi mkoani Kilimanjaro,linamshikilia mtumishi mmoja wa shirika moja la Umma mjini Moshi akituhumiwa kujihusisha na usafrishaji wa dawa za kulevya aina ya mirungi.

Kamanda wa polisi mkoani Kilimanjaro,Hamisi issah,amedhibitisha kukamatwa na kushikiliwa kwa mtumishi huyo ambaye kwa sasa tunahifadhi jina lake baada ya kukamatwa na shehena kubwa ya mirungi aliyokuwa akiisafrisha kwa kutumia gari lake dogo.

Mtumishi huyo alikamatwa desemba 19 mwaka huu nje kidogo ya mji wa Moshi baada ya gari lake kuparamia mti na kupata ajali akiwa katika jitihada za kuwakimbia polisi.

Kwa mujibu wa Kamanda Issah,dereva wa gari hilo alitimua mbio na kumwacha mtumishi huyo wa shirika la umma akitiwa mbaroni.

Taarifa zaidi pamoja na picha za mtuhumiwa huyo zitafuata hivi punde

Kwa taarifa juu ya mkasa huyo pamoja na majina kamili ya mtumishi huyo na taasisi anayofanyia kazi endelea kutembelea mtandao huu

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni