Alhamisi, 21 Desemba 2017

TAKUKURU YAFUNGA MWAKA KWA KISHINDO,YAPANDISHA VIGOGO SABA KORTINI KWA UFISADI NDANI YA SIKU TATU




NA CHARLES NDAGULLA,HAI

TAASISI  ya kuzuia na kupambana na rushwa mkoani Kilimanjaro(TAKUKURU) imetoa onyo kwa watumishi wa umma kuacha kuchezea fedha za serikali na atakayejaribu ataishia pabaya ikiwamo kufikishwa makahamani.

Onyo hili la Takukuru linakuja siku chache baada ya kuwafikisha makahamani watumishi saba wa Halmashauri ya wilaya ya Hai kwa tuhuma za kujihusisha na ufujaji wa fedha za umma.

“Takukuru tunasisitiza kuwa hakuna mbadhilifu wa fedha za umma mkoani Kilimanjaro atakayeabaki salama,ni suala la muda tu,hivyo ni rai yetu kuwa wenye fikra za kufanya ubadhilifu ni bora wakaacha mara moja na kujifunza kiridhika na vipato vyao halali au wakaacha kazi za umma wakatafute kazi zenye maslahi wanayodhani yatakidhi matamanio yao “,ni onyo la Mkuu wa takukuru,Holle Makungu

Watumishi hao wameshitakiwa kwa makosa ambayo yanafanana ya wizi na ubadhilifu na baadhi yao wamejikuta wakiburuzwa mahamani mara tatu kwa makosa hayo hayo ya ufujaji wa fedha za umma.

Aliyeanza kuonja joto ya jiwe ni Thadeus Theobald Meela ambaye alikuwa mweka hazi wa halmashauri hiyo wakati wa ufujaji wa fedha hizo kabla ya kuhamishiwa wilaya ya Ruangwa na baadaye Pangani mkoa wa Tanga.

Meela alijikuta akiunganishwa tena katika mashitaka ya wizi na ubadhilifu wa fedha hizo za umma  na Mkurugenzi wa Halmashauri ya mji wa Bariadi mkoani Simiyu ,Melkizedeck  Oscar Humbe pamoja na karani wa fedha,Valentina Elisha Mollel .

Watatu hawa wameshitakiwa kwa kosa la wizi na ubadhilifu wa zaidi ya shilingi Milioni 27wanaodaiwa kuufanya mwaka 2014 wakati huo Humbe akiwa Mkuregenzi wa halmashauri hiyo.

Takukuru katika kuonyesha haitanii,safari hii imemfikisha mahakamani Mganga mkuu wa Hospital ya Mkoa wa Kigoma(RMO) Dkt. Paul Christopher Chaote akishitakiwa na wenzake watano kwa makosa 109 ya ubadhilifu wa fedha wa zaidi ya shilingi Milioni 38  na kusaidia kutendeka kwa kosa pamoja na kuandaa nyaraka za uongo kwa lengo la kumdanganya mwajiri.

Wengine ni Philipo Alexander Masasi,Thadeus Theobald Meela,Christopher Nyamagera Manzi,Edwid Mtalemwa Kalokola na Valentina Elisha Mollel ambao wanadaiwa kutenda makosa hayo kati ya oktoba 2014 na januari 2015. 

Walifikishwa mbele ya hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya wilaya ya Hai,Arnold Kirekiano na kusomewa mashitka na waendesha mashitaka wa Takukuru,Rehema Mteta akisaidiana na Suzan Kimaro. 

Wanadaiwa kwa matumizi mabaya ya nyaraka ikiwamo kuandaa nyaraka za uongozi kwa lengo la kumdanganya mwajiri,ubadhilifu  na kusaidia kutenda makosa ambako wanadaiwa kutumbua kiasi hicho cha fedha zilizokuwa kwa ajili ya posho ya kuitwa kazini kwa madaktari(on Call allowance) katika hospital ya Machame .


Kwa mujibu wa hati ya mashitaka,washitakiwa hao wenaidaiwa kuwa,mnamo Oktoba mwaka 2014  kwa pamoja wakiwa watumishi wa halmashauri ya wilaya ya hai, kwa njia za udanganyifu walijimilikisha kiasi cha sh,Milioni 19.200,000 zilizokuwa kwa ajili ya posho ya kuitwa kazini kwa madaktari na wauguzi katika Hospital ya Machame.

Baada ya washitakiwa hao kuzitafuna fedha hizo ndipo walipoandaa nyaraka mbali mbali kuonyesha kuwa fedha hizo zililipwa kwa madaktari na wauguzi wa Hospital hiyo ya Machame kama posho ya kuitwa kazini kwa madaktari hao na wauguzi jambo ambalo halikuwa kweli . 

Baada ya kusomewa mashitaka hayo,washitakiwa Paul Chaote, Thadeus Meela, Valentina Molle na Christopher  Manzi walikana mashitaka yao  huku washitakiwa wengine wawili,Phillipo Alexander Masasi na Edwin Mtalemwa Kalokola wakiingia mitini .

Washitakiwa hao wapo nje kwa dhamana hadi Februari 15 mwaka 2018 kesi yoa itakapokuja kwa ajili ya kutajwa  baada ya kutimiza masharti ya dhamana yaliyowataka kila mmoja kuwa na wadhamini wawili wa kuaminika watakaosai bondi ya milioni 5, kila mmoja.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni