Jumanne, 12 Desemba 2017

MIILI YA WANAJESHI WA TANZANIA WALIOUAWA NCHINI DRC YAWASILI NCHINI

Miili ya wanajeshi wa Tanzania waliouawa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo(DRC) ikitolewa ndani ya ndege ya Umoja wa mataifa katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Jijini Dar es salaam jana desemba 11,2017

 Maofisa wa jeshi la wananchi wa Tanzania(JWTZ)wakiwa wamebeba moja ya jeneza lenye mwili wa askari wa jeshi hilo aliyekuwa miongozi mwa askri 14 waliouawa nchini Mamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo(DRC) alhamis ya desemba 7 mwaka huu mara baada ya kuwasili nchini jana jumatatu desemba 11


 Maofisa wa jeshi la wananchi Tanzania(JWTZ)wakiwa wamejipanga mstari tayari kuilaki miili ya askari 14 wa jeshi hilo waliouawa nchini DRC alhamis desemba 7 mwaka huu ilipowasili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa JKN Jijini Dar es salaam jana desemba 11

 Ndege ya shirika la Umoja wa Mataifa(UN)iliyobeba miili ya askari 14 wa jeshi la wananchi Tanzania(JWTZ)waliouawa nchini Kongo ikiwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es salaam jana desemba 11

 Miili ya askari 14 wa jeshi la wananchi Tanzania ikiingizwa kwenye gari la jeshi hilo muda mfupi baada ya kuwasili kutoka nchini DRC,askari hao wanadaiwa kuuawa na waasi wa ADF alhamis desemba 7 mwaka huu wakiwa katika kikosi cha kulinda Amani cha Umoja wa mataifa

 Umoja wa mataifa walaani shambulio dhidi ya walinda amani hao.


Miili ya wanajeshi 14 wa Tanzania waliouawa wakati wakihudumu katika kikosi cha Umoja wa Mataifa cha kulinda Amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imewasili jijini Dar es Salaam, Tanzania  jumatatu desemba 11.

Miili hiyo ilisafirishwa kwa Ndege za Umoja wa Mataifa kutoka nchini DR Congo na kupokelewa na maofisa wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania wakiongozwa na Waziri wa Ulinzi Hussein Mwinyi.

Waliuawa wakati wa shambulio lililotekelezwa Alhamisi ya desemba 7 mwaka huu  kwenye kambi ya jeshi ya Semuliki eneo la Beni katika mkoa wa Kivu Kaskazini.
Wanajeshi wengine zaidi ya 50 walijeruhiwa.

Umoja wa Mataifa ulisema wanajeshi 5 wa jeshi la DR Congo (FARDC) waliuawa pia kwenye shambulio hilo

Waasi wa ADF ndio wanaotuhumiwa kutekeleza shambulio hilo.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres alishutumu vikali shambulio hilo na kusema ni sawa na uhalifu wa kivita.

Aliitaka DR Congo kufanya uchunguzi kuhusu shambulio hilo na kusema kwamba waliohusika wanafaa kuwajibishwa.

Wanajeshi zaidi walitumwa eneo hilo na kamanda wa kikosi cha kulinda amani anaelekeza shughuli ya kuwaondoa majeruhi.

Bw Guterres alisema shambulio hilo ndilo mbaya zaidi kuwahi kutekelezwa dhidi ya walinda amani wa UN katika historia yake miaka ya karibuni.





 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni