Alhamisi, 21 Desemba 2017

KIWANDA CHA BANANA CHA D.G.T MOSHI KATIKA KASHFA


 Na Charles Ndagulla,Moshi

MAMLAKA  ya Chakula la Dawa(TFDA)Kanda ya kaskazini,imekifunga kiwanda cha kutengeneza pombe aina ya Banna inayotengenezwa na Kampuni ya Derrick Global Trading(D.G.T ) cha  mjini moshi kutoka na kubainika kuwa na kasoro .

Kiwanda hicho kimefungwa chini ya kifungu cha 181 sura ya 209 ya sheria ya chakula na dawa ya mwaka 2003 kutokana na tuhuma za kutumia nembo ya kiwanda kingine cha kutengeneza pombe kali kinyume cha sheria.

Akizungumza na waandishi wa habari kiwandani hapo,Mkaguzi wa chakula mwandamizi kutoka TFDA Kanda ya kaskazini,William Mhina,alisema sababu nyingine za  kufungwa kwa kiwanda hicho ni mazingira yasiyoridhisha ya kiwanda hicho.

Alitaja sababu zingine ni wafanyakazi kutokuwa na vyeti vya kuonyesha afya zao huku wafanyakazi hasa wa kike kutokuvaa kofia kichwani.

Alisema uchunguzi wao umebaini kuwa,eneo la kuoshea chupa ni chafu na kwamba chupa hizo zimekuwa zikioshwa katika mazingira yasiyoridhisha.

Alisema wamiliki wa kiwanda hicho wamepewa muda wa kurekebisha kasoro hizo na baada ya kufanya hivyo TFDA itafanya ukaguzi tena kujiridhisha kama kasoro hizo zimefanyiwa kazi,

Katika hatua nyingine,jeshi la polisi kwa kushirkiana na maofisa wa mamlaka ya mapato Tanzania(TRA),wamefanikiwa kukamata shehena ya vifungashio  vinavyotumiwa na kampuni moja mkoani Shinyanga  ya Canon General Supply inayojihusisha na utengenezaji wa pombe kali aina ya Shujaa.

Vifungashio hivyo vilikamatwa ndani ya kiwanda hicho kilichopo eneo la Kwa Alphone kata ya Kiborironi  huku baadhi ya wafanyakazi wa kiwanda hicho wakishikiliwa na jeshi la polisi kwa mahojiano zaidi.

Akizungumzia tukio hilo,ofisa huyo kutoka TFDA alisema hilo ni kosa kwa mujibu wa sheria inayosimamia usajili wa bidhaa na kuongeza kuwa,vifungashio vilivyokamatwa ndani ya kiwanda hicho havimo kwenye orodha ya usajili wa bidhaa zinazozalishwa na kampuni hiyo.


 Moja ya vifungashio vilivyokamatwa na polisi katika kiwanda cha D.G.T cha mjini Moshi,vifungahio hivyo ni mali ya Kampuni ya Canon General Supply ya mjini Shinyanga.

 Kwa upande wake kamanda wa polisi mkoa wa Kilimanjaro,Hamisi Issah alisema jeshi hilo linamshikilia meneja wa Kiwanda hicho aliyemtaja kwa jina la Boniface Damas(56) pamoja na wafanyakazi watatu wa kiwanda hicho.
Kamanda Issah aliwataja wafanyakazi hao kuwani Severine Pantaleo(37),Riziki Fabian (28) na Daniel Japhet(18) ambao wanadaiwa kukutwa na pombve kali iliyofungashwa kwenye viroba iana ya Zed inayodaiwa kutengenezwa kienyeji.

“Viroba hivyo vina alama zake,lakini watuhumiwa hawa walikuwa wakitengeneza katika mfumo wanaoujua wenyewe,utengenezaji wa pombe usiozingatia taratibu ni hatari na unaweza kuleta madhara makubwa kwa wanywaji”,alisema kama Issah.

Kuhusu vifungashio vilivyokamatwa ndani ya kiwanda cha D.G.T,kamanda Issah alisema kuwa,wamiliki wa kiwanda hicho hawakuwa na haki stahiki ya kutengeneza pombe hizo kutokana na kutengeneza pombe hizo pasipo kuzungitia tararibu za kisheria.

Kamanda Issah amesema polisi kwa kushirikiana na TFDA wanafanya uchunguzi juu ya tuhuma hizo ikiwamo matumizi ya malighafi isiyo ya kiwanda hicho na uchunguzi ukimalika shweria itachukua mkondo wake kwa watakaobainika kutenda makosa.
 
 Meneja wa Kiwanda cha Derrick Global Trading(D.G.T) cha mjini Moshi,Boniface Damas(kulia)akiwa ndani ya gari la polisi na watuhumiwa wenzake baada ya kukamatwa kwa tuhuma za kutengeza pombe kali kwa kutumia vifungashio vya kampuni ya Canon General Supply ya mjini Shinyanga kinyume cha sheria.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni