Alhamisi, 28 Desemba 2017

MTUMISHI WA MFUKO WA PENSHENI KWA WATUMISHI WA UMMA PPF ALIYENASWA NA SHEHENA YA DAWA ZA KULEVYA AENDELEA KUSOTA RUMANDE

Mtuhumiwa wa dawa za Kulevya aina ya Mirungi,Anitha Osward ambaye ni mtumishi wa Mfuko wa Pensheni kwa watumishi wa umma(P P F) mkoani Kilimanjaro akiwa chini ya ulinzi wa polisi baada ya kukamatwa akituhumiwa kusafrisha shehena ya dawa za kulevya,alikamatwa Desemba 19,2017 eneo la Majengo kwa Mtei mjini Moshi.
 Anitha Osward mkazi wa karanga Manispaa ya Moshi ,mtuhumiwa wa dawa za kulevya akiwa haamini kilichotokea baada ya kukamatwa na makachero wa polisi akituhumiwa kujihusisha na usafrishaji wa dawa za kulevya aina ya mirungi.
 Shehena ya mirungi ikiwa kituo cha polisi baada ya kukamatwa ikisafrishwa ndani ya gari aina ya Toyota Sienta lenye namba za usajili T674 DLB linaloaminika kumilikiwa na mtumishi wa mfuko wa Pensheni kwa watumishi wa umma(P P F),Anitha Osward.
 Shehena ya Mirungi ikiwa ndani ya gari lenye namba za usajili T674 DLB aina ya Toyota Sienta baada ya kukamatwa na polisi hivi karibuni eneo la Majengo Kwa Mtei nje kidogo ya mji wa moshi.
 Gari aina ya Toyota Sienta lenye namba za usajili T674 DLB likivutwa baada ya kupata ajari eneo la Majengo kwa Mtei mjini Moshi,gari hilo lilikamatwa na polisi likiwa na hsehena ya dawa la kulevya aina ya Mirungi.
 Gari aina ya Toyota Sienta lenye namba za usajili T674 DLB likiwa kituo cha polisi mjini moshi baada ya kukamatwa likiwa na kilo 216 na gramu 370 za dawa kulevya aina ya mirungi .
 Kama inavyyonekana nyuma ya buti ya gari lenye namba za usajili T674 DLB aina ya Toyota Sienta ni shehena ya dawa za kulevya aina ya mirungi baada ya kukamatwa na polisi hivi karibuni ikisafrishwa na mtumishi wa shirika la umma(P P F),Anitha Osward.




 TAARIFA YA JESHI LA POLISI KILIMANJARO JUU YA KUKAMATWA KWA SHEHENA YA DAWA ZA KULEVYA IKISAFRISHWA NA MTUMISSHI WA MFUKO WA PENSHENI KWA WATUMISHI WA UMMA(P P F) ANITHA OSWARD.


JESHI la polisi mkoani Kilimanjaro, linamshikilia mfanyakazi mmoja wa mfuko wa pensheni kwa watumishi wa umma(PPF) kwa tuhuma za kujihusiha na usafirishaji wa dawa za kulevya. 


Mtumishi huyo,Anitha Osward(32)alikamatwa desemba 19 mwaka jana akiwa na shehena ya madawa ya kulevya aina ya mirungi aliyokuwa akiisafrisha kwa kutumia gari lake dogo aya ya Toyota Sienta lenye namba za usjaili T674DLB.

 Kwa mujibu wa kamanda wa polisi mkoani Kilimanjaro,Hamis Issah,mtuhumiwa huyo ambaye bado anashikiliwa na jeshi la polisi mpaka sasa,alikamatwa na askari waliokuwa doria.

“Askari wakiwa doria walimkamata Anitha Oswald, ambaye ni mkazi wa Karanga, Manispaa ya Moshi, akiwa anasafirisha dawa za kulevya aina ya mirungi kilo 216 na gramu 370”, alisema kamanda Issa. 

Kamanda Issa alisema Anitha Oswald alikamatwa eneo la Majengo kwa Mtei Disemba 19, mwaka jana, akiwa anatokea Njia Panda ya Himo kuchukua mzigo huo. 

Aidha kamanda Issa alisema kwamba usafirishaji wa dawa za kulevya bado ni changamoto kubwa ambapo alielezea kusikitishwa na tabia ya baadhi ya watumishi wa Umma kujihusisha na usafirishaji huo.

“Jeshi la polisi mkoani hapa liko makini, operesheni inaendelea na hatutamvumilia mtu yeyote ambaye atabainika kujihusisha na biashara hii”, alisema.

Hata hivyo kamanda aliongeza kusema kwamba jeshi hilo la polisi mkoni kilimanjaro, bado linaendelea kumtafuta dereva wa gari hilo, ambaye alikimbia baada ya kulitelekeza gari alilokuwa akiliendesha baada ya kugonga mti katika jitihada za kuwakimbia polisi.


 imeandaliwa na Charles Ndagulla,Moshi










Hakuna maoni:

Chapisha Maoni