Jumanne, 21 Novemba 2017

TRA YAZIFUNGA AKAUTI ZA MAMLAKA YA MAJI MOSHI MJINI MUWSA




RUNGU la mamlaka ya mapato Tanzania(TRA) kufunga akaunti za walipakodi wakorofi  na kukamata mali zao limeikumba  Mamlaka ya Maji safi na maji taka Moshi Mjini(MUWSA) ambako akaunti za mamlaka hiyo zinadaiwa kufungwa.

Kufungwa kwa akaunti za mamlaka hiyo kulikodhibitishwa na mkurugenzi wake Joyce Msiru  ni kutokana na madai kwamba mamlaka hiyo inadaiwa shilingi Bilioni 2.6 ikiwani malimbikizo ya kodi mbali mbali.

Hata hivyo mkurugenzi  huyo wa MUWSA Joyce Msiru anapinga deni hilo akidai baadhi ya kodi zilizoanishwa na TRA hawawezi kuzilipa kutokana na wao(mamlaka) kutojiendesha kibiashara huku akidaia TRA imesisitiza lazima madeni hayo yalipwe.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka TRA,kiasi hicho cha deni ni kutokana na ukaguzi uliafanywa kati ya mwaka 2013 hadi mwaka jana ambsalo linahusisha kodi mbali mbali ikiwmao VAT,Corporation tax,Skillls Development Levy na nyinginezo.

Mkurugenzi huyo amesema mamlaka yake haiwezi kulipa kodi ya Coporation tax inayofikia shilingi Milioni 847 kutokana na kile alichodai mamlaka yake haifanyi biashara badala yake inategema mapato kutokana na Ankara za maji kutoka kwa wateja.

“Mfano hiyo kodi ya coporation tax wanayotudai hiyo ni kodi inayolipwa na makampuni au taasisi zinazojiendesha kibiashara lakini sisi MUWSA income yetu inatokana na Ankara za maji zinazolipwa na wateja,sasa hapo sisi tunahusikaje?”,alihoji.

Kuhusu shilingi Milioni 948 ambazo  TRA inaidai MUWSA kama kodi ya ongezeko la thamani(VAT) mkurugenzi hiyo amedai kuwa kuna mkanganyiko mkubwa katika kutafsiri sheria kutokana na kwamba kwenye maji sheria imesamehe VAT lakini kwenye huduma ya majitaka sheria imekaa kimya.

Kodi nyingine ambayo mamlaka hiyo wanadai hawastahili kulipa na ambayo TRA wamesisitiza lazime ilipweni ya Skills Development Levy ambako wanadaiwa shilingi milioni 569.

Akizungumzia kodi hiyo,mkurugenzi huyo anadai kuwa mwaka 2012 TRA waliirejeshea mamlaka hiyo kiasi cha shilingi milioni 39 baada ya kutozwa na mamlaka hiyo katika mwaka 1999 na 2002 na kuhoji iweje kodi hiyo  irejeshwe tena kwa mamlaka yake.

Kutokana na mvutano huo ,mkurugenzi huyo amedai kuwa kwa sasa sakata hilo limepelekwa kwa katibu mkuu wa wizara ya maji,profesa Kitila Mkumbo kwa ajili ya kulitafutia ufumbuzi huku taarifa zikipasha kuwa sakata hilo sasa limeziunganisha wizara mbili,wizara ya maji na wizara ya fedha.

Mbali na kupelekwa huko,mkurugenzi huyo ameliambia Jamhuri kuwa imeundwa timu  itakayoshughulikia madai ya mamlaka za maji kote nchini ambako inadaiwa kuwa zimekuwa zikitozwa kodi na TRA kadri wanavyoona.

“Lengo letu tunataka kuwe na mfumo unaoeleweka wa utozwaji kodi kwa mamlaka zote nchini tofauti na sasa ambako utasikia mamlaka hii wanatozwa kodi fulani,sasa huu mkanganyiko tunataka tuumalize”,alisema.

Kutokana na kufungwa kwa akaunti za mamlaka hiyo,wafanyakazi kadhaa wa mamlaka hiyo walijawa na hofu ya kukosa mishahara yao ya mwezi oktoba lakini taarifa zilizopatikana baadaye na kudhibitishwa na mkurugenzi huyo,TRA imeregeza kamba na kuzifungua huku ikitishiak uzifunga tena kama hakitaeleweka.

WADAIWA SUGU MUWSA NAO KUKIONA CHA MOTO

Wakati Mamlaka hiyo ikitikiswa kwa akaunti zake kufungwa na TRA na baadaye kufunguliwa kwa masharti,mkurugenzi huyo amesema kuwa,mamlaka yake bado inasaka dawa ya kuondoka na wadaiwa sugu wa mamlaka hiyo.

Amesema hadi sasa wanazidai taasisi za serikali ikiwamo ofisi ya kamanda wa polisi mkoa wa Kilimanjaro,Chuo cha taaluma ya polisi(MPA) na Magereza mkoa zaidi ya shilingi Bilioni 1.7.

Amesema pamoja na kuzikatia huduma ya maji taasisi hizo na baadaye kuzirejeshea huduma hiyo,hakuna dalili zozote za kulikwa kwa malimbikizo hayo ya Ankara za maji kutokana na wakuu wa taasisi hizo kudai hawana pesa.

“Tunaona suluhisho la yote haya ni kuwafungia mita za maji ili  kubaini kiwango cha matumizi yao na sasa tupo katika hatua za mwisho kukamilisha mchakato huo na tunaamini tukifanya hivyo tutakuwa tumekata mzizi wa fitina”,alisema.

Mara kwa mara mamlaka hiyo imekuwa ikichukua hatua za kusitisha huduma ya maji safi kwa taasisi hizo za serikali kutokana na ukubwa wa malimbikizo ya madeni hayo lakini huishia kuendelea kutoa huduma kutokana na unyeti wa taasisi hizo.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni