Jumamosi, 25 Novemba 2017

VIPIMO VYA DNA VYAKWAMISHA MAZISHI YA MWANAFUNZI WA SCLOLASTICA HIGH SCHOOL

Askari wakishirikiana na ndugu wa marehemu Humphrey Makundi kufukua kaburi ulimozikwa mwili huo katika makaburi ya Karanga mjini Moshi hivi karibuni baada ya mahakama ya hakimu mkazi mjini Moshi kutoa kibali cha kuufukua mwili huo kwa ajili ya kuufanyia uchunguzi.


Baba mzazi wa marehemu Humphrey makundi ,Jackson Makundi(katikati)akijadili jambo na ndugu zake wakati zoezi la kuufukua mwili wa mwanaye likiendelea katika makaburi ya Karanga mjini Moshi hivi karibuni. 



Na Charles Ndagulla,Moshi

MAZISHI  ya mwanafunzi,Humphrey Makundi(16) wa shule ya Sekondari ya Scolastica iliyopo katika mji mdogo wa Himo anayedaiwa kupigwa na kitu chenye ncha kali,yamekwama kufanyika jumamosi hii.

Kukwama kwa mazishi hayo kunatokana na kuchelewa kutoka kwa majibu ya vipimo vya vinasaba(DNA)vilivyopelekwa kwa mkemia mkuu wa serikali na sasa mazishi hayo yatafanyika wiki ijayo.

Akizungumza na waandishi wa habari wiki hii mjini hapa,Baba mzazi wa marehmu,Jackson Makundi alisema kuwa wanatarajia kupata majibu ya vipimo hivyo wiki ijayo na baada ya kutoka kwa majibu hayo,tararibu za mazishi zitafanyika mapema iwezekanavyo.

“Tunaomba uchunguzi ufanyike haraka na majibu ya vipimo yatoke haraka ili niweze kumzika kwa heshima mtoto wangu,kwakweli ameteseka sana”,alisema makundi katika mkutano wake na vyombo vya habari.

Mwanafunzi huyo aliyekuwa akisoma kidato cha pili katika shule hiyo,anadaiwa kutoweka shuleni hapo asubuhi ya Novemba saba na mwili wake kupatikana Novemba 10 ukiwa ndnai ya mto Wona mita 300 kutoka shule hapo.

Mwili huo unadaiwa kukutwa na majeraha kichwani hali inayodhihirika kuwa kabla ya kifo chake marehemu aliteswa kwa kupigwa na kitu kizito kilichopasua fuvu lake.

Baba mzazi wa marehemu alisema katika mkutano wake na wanahabari kuwa,kwa mujibu wa taarifa aliyopewa na daktari aliyeufanyia uchunguzi mwili huo,mwanye alipigwa na kitu chenye ncha kali na kupasua fuvu na kukana taarifa zinazoenezwa kuwa alikufa kwa maji.

Hadi sasa jeshi la polisi linawashilia zaidi ya watu 11 kwa mahojiano akiwamo mmiliki wa shule hiyo,Edward Shayo wakituhumiwa kuhusika na mauaji hayo ambayo yameutikisa mji wa Himo na mkoa mzima wa Kilimanjaro.

Mauji hayo pia yamelaaniwa na baadhi ya wazazi wenye watoto wanaosoma katika shule mbali mbali za bweni huku wakitilia shaka usalama wa watoto wao na kuzitaka mamlaka husika kufanya uchunguzi wa kina juu ya tukio hilo na kuwafikisha mahakamani watakaobainika kutenda unyama huo.

Wengine wanaoshikiwa yumo mlinzi wa shule hiyo anayedaiwa kumpiga na kitu kizito marehemu,wamo daktari katika hopsital ya mkoa,mawenzi wanaodaiwa kufanya udanganyifu kuhusu umri wa marehemu na kutoa kibali cha kuuzika mwili huo chap chap.



 

Maoni 1 :

  1. Kwani hii blog bado inafanya kazi ndagula, naomba tutumie habari bwana, Stambuli- 0655339616

    JibuFuta