Jumatatu, 27 Novemba 2017

MMILIKI WA SHULE YA SEKONDARI SCOLASTICA APIGWA PINGU

Ama kweli sheria ni msumeno,pichani Edward Shayo,mmoja wa wamiliki wa shule ya Sekondari Binafsi ya Scolastica iliyopo Himo mkoani Kilimanjaro,akiwa amepigwa pingu muda mfupi baada ya kutoka kwenye chumba cha mahabusu kilichopo mahakama ya hakimu mkazi,Shayo na wenzake wawili wamesomewa shitaka la mauaji ya mwanafunzi wa shule hiyo,Humphrey Makundi.
Jengo la mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi ambako washitakiwa wa mauaji ya mwanafunzi Humphrey Makundi wa kidato cha pili katika shule ya Sekondari Binafsi ya Scolastica iliyopo mji mdogo wa Himo Mkoani Kilimanjaro walisomewa shitaka la mauaji ya mwanafunzi huyo.

Hili ndilo kaburi ambalo linadaiwa kuzikwa  mwili wa marehemu Humphrey Makundi mwanafunzi wa kidato cha pili katika shule ya sekondari Binafsi ya Scolastica iliyopo katika mji mdogo wa Himo Mkoani Kilimanjaro anayedaiwa kuuawa na mlinzi wa shule hiyo Novemba 6 mwaka huu na mwili wake kutupwa mto Wona mita 300 kutoka shuleni hapo,mwili huo ulizikwa makaburi ya Karanga Mjini Moshi kabla ya kufukuliwa Novemba 17 baada ya mahakama ya hakimu mkazi kutoa kibali cha kuufukua



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni