Ijumaa, 2 Januari 2015

36 WAPOTEZA MAISHA SIKUKUU YA MWAKA MPYA, ‘SHANGHAI STAMPEDE’



Watu 36 wamepoteza maisha na wengine kiasi ya 40 kujeruhiwa kutokana na mkanyagano katika hekaheka za kusherehekea mwaka mpya nchini China.

Tukio hilo lilitokea wakati umati mkubwa wa watu ukiwa umekusanyika katika uwanja wa Chen Yi Square. Shirika la habari la China Xihnua limemnukuu aliyeshuhudia mkasa huo akisema watu walikuwa wakitaka kujipatia kuponi ambazo zilionekana kama fedha aina ya dola ambazo zilikuwa zikirushwa kutoka katika dirisha kutoka gorofa ya tatu ya jengo moja.

Serikali ya China iliosema umma huo wa watu ulianza kukanyagana mapema kabla ya kutimia usiku wa manane, katika mji huo wenye mchanganyiko wa watu. Tukio hilo linaelezwa kuwa baya zaidi kutokea tangu mwaka 2010, baada ya kuzuka moto katika jengo lenye makazi ya watu na kusababisha vifo vya watu 58.

Chanzo cha mkanyagano huo bado hakijafahamika lakini chombo cha habari cha serikali na baadhi ya walioshuhudia wanasema kwa sehemu fulani kadhia hiyo imesababishwa na watu wakiwania kujipatia fedha zilizoonekana kama ni sarafu halisi.

 CHANZO: DW

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni