Rais wa Marekani Barack Obama
ameahidi kuisadia Mexico dhidi ya wimbi la machafuko na magenge ya walanguzi wa
dawa za kulevya.
Obama alikutana na rais wa
Mexico Enrique Pena Nieto katika ikulu yake mjini Washington jana huku kukiwa
na wasiwasi kuhusiana na kutekwa kwa wanafunzi 43 wa Mexico mwezi Septemba
mwaka uliopita.
Waandamanaji kadhaa
walikusanyika nje ya ikulu wakitaka kujua kilichotokea kwa wanafunzi hao ambao
inachukuliwa walikufa wakiwa mikononi mwa viongozi na maafisa wa polisi
wanaoshirikiana na genge la walanguzi wa dawa za kulevya.
Obama alikabiliwa na shinikizo
kutoka kwa makundi ya haki za binadamu likiwemo Human Rights Watch kumshinikiza
Pena Nieto atilie maanani zaidi suala hilo la wanafunzi.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni