HAJIBU AKIBANWA MBAVU
NA WALINZI WA MBEYA CITY FC.
Timu ya soka ya Simba jana ilikwaa kisiki katika michuano ya ligi kuu ya Tanzania Bara baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa Mbeya City.
Katika mechi hiyo iliyochezwa
kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Simba ilikuwa ya kwanza kupata bao
dakika ya 23 lililofungwa na mshambuliaji chipukizi Ibrahim Ajibu. Bao hilo
lilidumu hadi mapumziko.
Mbeya City ilisawazisha bao
hilo dakika ya 76 kupitiakwa Paul Nonga baada ya kufanyika kwa shambulizi kali
kwenye lango la Simba.
Bao la pili na la ushindi la
Mbeya City lilifungwa kwa njia ya penalti na Yussuf Abdalla baada ya kipa
Manyika Peter wa Simba kudaka mguu wa Raphael Alfa ndani ya mita 18 badala ya
mpira.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni