ALVARO RODRIGUEZ
Mkurugenzi
Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa, Alvaro Rodriguez amesema Umoja wa Mataifa
(UN) umesikitishwa na kitendo cha kuporwa kwa mtoto mwenye ulemavu wa ngozi,
Pendo Emmanuel (4) na watu wasiojulikana kilichotokea katika kijiji cha Ndami
wilayani Kwimba mkoani hapa ambapo hadi sasa bado hajapatikana.
Katika
mkutano wake na waandishi wa habari uliofanyika jijini Mwanza baada ya
kutembelea mikoa ya Kanda ya Ziwa ikiwemo Mara, Shinyanga na Mwanza kuangalia
miradi inayotekelezwa na Umoja wa Mataifa pamoja na masuala ya haki za binadamu,
Alvaro Rodriguez alisema serikali kupitia Mkuu wa mkoa, Magesa Malongo na
Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza, Valentino Mokiwa wahakikishe wanaendelea
kumtafuta na kulipa suala hilo kipaumbele.
Hadi
kufikia jana zilikuwa zimefika siku 13 tangu mtoto huyo aporwe na watu
wasiojulikana Desemba 27, mwaka jana katika kijiji cha Ndami, tarafa ya
Mwamashinda wilayani Kwimba.
Kwa
upande wake, Kamanda Mlowola alisema licha ya jitihada zinazofanywa na Jeshi la
Polisi za kumtafuta mtoto Pendo, lakini bado hajapatikana. wa mkoa wa Mwanza,
Magesa Mulongo mwanzo mwa wiki hii alitoa siku tano kwa uongozi wa kijiji cha
Ndami, wilayani Kwimba na Jeshi la Polisi kuhakikisha wanampata mtoto huyo hadi
ifikapo leo.
Tayari
watu 15 wanashikiliwa na polisi kwa uchunguzi zaidi wa kuhusika na uporwaji wa
mtoto huyo akiwemo baba mzazi, Emmanuel Shilinde.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni