Jumanne, 27 Januari 2015

KAMBI YA WAZEE WASIOJIWEZA MOSHI YAGEUKA JEHANAMU



Wazee wasiojiweza wanaoishi kwenye kambi ya wazee ya Njoro katika Manispaa ya Moshi inayomilikiwa na serikali kuu  wanakabiliwa na matatizo mbali mbali ikiwa ni pamoja na ukosefu wa huduma za afya,usafiri na uzio wa makazi yao.
 MZEE INYASI ATANASI
 MATHAYO MAYUNGA


 Bi. NDETA TENGA

Wazee hao wametoa malalamiko  hayo kwa kikundi cha familia ya wakazi wa Manispaa ya Moshi cha ‘Big Family’ ambao waliitembelea kambi hiyo kuwapa misaada ya kijamii wazee hao na kula nao chakula cha mchana.
Wakizungumza kwa niaba ya wenzao Mzee Salim Ali na Mzee Inyasi Atanasi ambaye ni mwenyekiti wa wazee hao wamesema, ingawa kuna zahanati katika kambi hiyo lakini haina dawa za kutosha na hamna vipimo wanapougua..
Malalamiko ya wazee hao yameungwa mkono  na Afisa Ustawi Mfawidhi wa kambi hiyo yenye uwezo wa kuhudumia wazee 35 Bi. Ndeta Tenga na kueleza kuwa  wazee wanne wamefariki dunia  kati ya mwezi Januari na Mei mwaka jana na kuiomba serikali iboreshe huduma za kambi hiyo.

Akiongea na wazee hao baada ya kukabidhi msaada huo ukiwemo unga, nguo,mafuta ya kupikia, mchele, sukari, sabuni na viatu vyenye thamani ya zaidi ya shs. 2.5mil/= Mwenyekiti wa ‘Big Family’ Dismas Dede ameahidi kuboresha baadhi ya huduma ikiwa ni pamoja na kukarabati jiko.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni