ZITTO KABWE
Kamati
ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kesho itawasha moto upya bungeni wakati
itakaposoma ripoti maalumu ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali
(CAG), ikitarajiwa kuibua kashfa tatu nzito ikiwamo ya misamaha ya kodi.
Kashfa
nyingine zinazotarajiwa kuibuliwa kesho ni, ufisadi katika gharama za ujenzi wa
jengo la watu mashuhuri (VIP) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius
Nyerere (JNIA) na uuzaji wa nyumba ya Bodi ya Korosho.
Akithibitisha
Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe zilisema
kuwa, tayari kamati hiyo imepokea ripoti ya ukaguzi huo ambayo inaonyesha
ufisadi wa kutisha katika maeneo hayo matatu na mengineyo.
Masuala
hayo matatu pia yaliibuka wakati wa vikao vya kamati za Bunge vilivyomalizika
Dar es Salaam wiki iliyopita, huku bodi ya korosho ikibanwa kuhusu nyumba yake
aliyouziwa Mbunge wa Kibaha Mjini (CCM), Silvestry Koka.
Kwa
mujibu wa habari hizo, ripoti hiyo inayoonyesha jinsi ufisadi wa kutisha
ulivyofanywa katika ujenzi wa jengo la (VIP Lounge) na Serikali inadai ilitumia
Sh12 bilioni kulijenga, lakini mthamini wa majengo ya Serikali ameeleza kuwa
jengo hilo lina thamani ya Sh3 bilioni.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni