Mshambuliaji wa Yanga, Amis Tambwe, akiwa chini akijilaumu baada ya
kukosa bao la wazi katika mchezo wa Robo fainali ya Kombe la Mapinduzi uliochezwa
jana kwenye uwanja wa Aman mjini
Zanzibar.
Katika mchezo huo JKU ilishinda kwa bao 1-0 lililofungwa na Amour Omary
katika dakika ya 72.
Kwa matokeo hayo sasa Yanga ni timu ya tatu kuaga mashindano hayo
ikiungana na Azam FC, iliyofungwa na Mtibwa Sugar na KCCA iliyofungwa na
Polisi, ambapo sasa JKU itakutana na Mtibwa Sugar katika hatua ya nusu fainali.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni