DIDIER DROGBA AKIWADHIBITI WALINZI WA LIVERPOOL 2009
Jose Mourinho alikuwa akiingia
katika soka la England, na kukutana na hali ambayo aliitumia fursa muhimu kwa
ajili ya kujipatia ujiko; hii ilikuwa ni michuano ya ligi ikiwa chini ya
mdhamini Carling.
Wengi waliitazama michuano ya
Carling Cup kama ‘Kombe la Mbuzi’ isiyo na maana yoyote ile kwao, alimpapatua
Sir Alex Ferguson kisha Rafa Benitez akiwa Liverpool aliidungua mabao 3-2.
Katika dakika ya kwanza,
utamkumbuka John Arne Riise wa Liverpool alitupia bao; lakini hali ilibadilika
ghafla Steven Gerrard alipojifunga bao na kuipa ahueni ‘the blues’ hadi muda wa
nyongeza ambako Chelsea iliwatungua Liverpool mabao matatu.
Nyota wa Liverpool Anntonio Nunez
alitupia bao katika dakika ya 113, lakini bao lake lilikuja mwishoni
wakati Didier Drogba na Mateja Kezman
walipotupia mabao.
CHANZO:
JAIZMELALEO
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni