Alhamisi, 8 Januari 2015

POLISI UFARANSA YAZIDI KUWASAKA MAGAIDI WALIOVAMIA ‘MEDIA HOUSE’ JIJINI PARIS


Polisi wa kupambana na ugaidi wa Ufaransa wameanzisha operesheni ya kuwasaka washambuliaji waliowaua watu 12 katika ofisi za jarida la kila wiki la Chalie Hebdo mjini Paris jana. 

Waziri mkuu wa Ufaransa Manuel Valls amesema watu kadhaa wamekamatwa. 

Televisheni za Ufaransa zimewaonyesha walenga shabaha wa kikosi maalumu cha polisi wakiwa katika barabara za mji wa Reims, huku duru zilizo karibu na operesheni hiyo zikisema wanaume watatu, wawili kati yao wakiwa ndugu, wametambuliwa kama washukiwa. Polisi wametoa picha za ndugu hao. 

Mmoja wa washukiwa hao watatu alifungwa jela mwaka 2008 kwa kuhusika na mtandao unaowapeleka wapiganaji nchini Iraq. Washukiwa wanasemakana kuwa na umri wa miaka 18, 32 na 34.

Taarifa za hivi karibuni zimeeleza kuwa mmoja wa washukiwa hao amejisalimisha kwa polisi. Zaidi ya watu 100,000 walijitokeza kote Ufaransa kuyapinga mauaji hayo. 

Rais wa Ufaransa Francoise Hollande amelieleza shambulizi hilo kuwa la kigaidi na kutangaza leo kuwa siku ya maombolezo ya kitaifa.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni