Jumamosi, 10 Januari 2015

PARIS SASA SHWARI, MAGAIDI WAUAWA



Majeshi ya usalama nchini Ufaransa, jana Ijumaa yakitumia mabomu na bunduki yalifikisha mwisho siku tatu za ugaidi mjini Paris, wakiwauwa ndugu wawili wenye mahusiano na kundi la al-Qaeda.
Ndugu hao walifanya mauaji ya watu 12 katika jarida la vikatuni vya dhihaka la Charlie Hebdo na mtu mwingine ambaye alishiriki katika mauaji hayo aliwakamata mateka watu kadhaa katika duka la Wayahudi akijaribu kuwasaidia ndugu hao kutoroka.

Ghasia mbaya kabisa za kigaidi nchini Ufaransa kuonekana kwa miongo kadhaa zimesababisha kuuwawa kwa kiasi ya watu 20, ikiwa ni pamoja na watu hao watatu waliokuwa na silaha. Mshukiwa na nne, mke wa mtu aliyeshambulia katika eneo la soko, bado anatafutwa na anaaminika kuwa ana silaha.

Kesho Jumapili kutakuwa na mkusanyiko mkubwa mjini Paris kuwakumbuka wahanga wa shambulio hilo ambapo viongozi kadhaa watahudhuria.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni